Alizaliwa
1948
Kingston
Jamaica
Mtindo
ska
Miaka
aliyofanya kazi 1963-1965
Lebo
Studio one
Jambo moja linalojulikana kimakosa na
wengi wa mashabiki na wapenzi wa muziki wa reggae, kuna Wailer asili mmoja tu
aliyehai (aliyebaki) lakini hiyo si kweli.Na wailer mwenyewe anatatubulika kama
Neville O’riley Livingstone. Anajulikana vizurI kama Bunny Wailer lakini Beverly
kelso ni msingi na jiwe kuu la pembeni la The Wailers bado anaishi. Anaishi Brooklyn,New York.
Alizaliwa
Kingston Jamaica mnamo mwaka 1948 na alisoma shule ya Nembhard Pre na baadaye
Denham Town Primary School, Kingston
Ingawa
hatajwitajwi sana lakini ana mchango mkubwa sana katika kujenga msingi imara uliowafanya
Bob Marley na The Wailers kuwa maarufu duniani.Akihusika kwa namna nyingi
katika Maendeleo ya kundi
Uwezo wa
kelso unaweza kuupata katika nyimbo alizoshiriki kuitikia (backing vocal ) na
kusaidia kutia mvuto. Baadhi ya nyimbo alizoshiriki ni Simmer Down, It hurts to
be alone na Lonesome feeling.
Ilikuwa
jumatatu angavu jioni mwishoni mwa mwaka 1963 ambapo vijana watano chini ya
miaka ishirini (20) Robert Nesta Marley, Neville livingstone, Winstone Hubert
Macintosh, Junior Brathwaite na msichana pekee katika kundi Beverly kelso
waliingia katika mlango wa nyumba namba 13 Brentford road Kingston 5 (baadaye
ilijulikana kama Studio One ) kwa
matumaini ya kutengeneza historia katika
muziki, walikuwa na nyimbo nne,Simmer Down, Idon’t need you love, How many
times na Straight and narrow way, sauti ya Kelso ikisikika katika kila wimbo.Kwa
msaada wa sauti za nyimbo waliupata kutoka bendi ya skatalites, The Wailers
wakafanikiwa kutoa wimbo wa Simmer Down ambao ulipata umaarufu mwanzoni mwa
mwaka 1964 na kushika chati namba moja kwa wiki kadhaa.
Sauti
nzuri ya juu ya Kelso ikitikia (Background Vocals) ikitoa mlingano mzuri kwenye
kundi,ikaacha athali chanya na kulifanya
kundi liifanye alama ya sauti ya kundi.
- Bob Marley,Bunny Wailer,Beverly Kelso na Peter Tossh
Sauti
ya juu ya Kelso inasikika vizuri zaidi kwenye nyimbo za Simmer Down na Lonesome
feeling baadaye alitoa mchango mkubwa katika kuingiza matumiziya kinanda cha
upepo (Pumping Organ) msaada ukiupata katika bendi ya Viking, kinanda hicho
unaweza kukisikia katika nyimbo nyingine kama Cyrus na there‘s A Reward za Joe
Higgs na Roy Wilson.
Akizungumza
kutoka New York yaliko makazi yake, anasema alirekodi nyimbo ishrini na tano
(25) na kundi kabla hajaondoka mwishoni mwa mwaka 1965 ukiwemo mmoja ulio na
jina Let the lord be seen in you. Kuondoka
kwake kuliliacha kundi pweke. Walikwenda mbali zaidi na kumtungia wimbo
ilioitwa Donna.
Robert Nesta Marley na Rita Anderson
Akizungumza katika Tribute to the Great mwaka 2012, alisema kulikuwa na mjadala mkubwa katika kundi kuhusu masuala yanayohusu mwelekeo wa kundi lililokuwa linakuwa kwa kasi pamoja na jitihada kubwa zilifanyika kujaribu kumshawishi abadili mawazo yake ya kuondoka.
Kulingana
na maelezo yake alibaki akiheshimiwa kukubaliwa na wengi kila kuthaminiwa na
wengi kila kundi lilipohusika.
Wakati
Marley anamuoa Rita Anderson, February 10, 1966, Kelso ni mtu pekee katika
kundi aliyekuwa najua. Aliyasema hayo wakati wa mahojiana na Colby Graham, mhariri
wa jarida la Vintage Boss.
Kelso
alikuwa ufunguo muhimu tena katika kundi la The Wailers pale alipomtambulisha
Rita Anderson kwa Clement “Coxson“Dodd. Ushirikiano huo sio tu ulimwingiza Rita
katika biashara ya muziki bali pia ulifungua milango ya mahusiano na Bob
Marley.Unaweza kusema,bila kujua alinzisha ujenzi wa himaya ya Marley . kwenye
nahojiano ya mwaka 2004 mjini New York na jarida la Vintage Boss kelso
alieleza.
“Wakati
tunaenda Studio kutoka Trench Town mara
kwa mara tulipita njia ya mkato kupitia Ninth Street na makaburi ya Calvary
tukipita nyumbani kwa akina Rita. Mara nying alikuwa na mtoto mikononi, na mara
nyingi akitupungia mkono. Wengine walimpuuza lakini kama mwanamke nilijisikia
vibaya nikawasimamisha, hawakupenda, siku moja mchana akaniambia ana wimbo
aliouita “Opportunity” anataka kurekodi, nilimweleza bwana Dodd na akasema nimlete.nilimfuata
lakini hakuwa amejiandaa.Mpaka awatafute waitikiaji wake (Backing Singers)
mmoja tulimwita Dream na mwingine tulimwita Precious, wakipita Soulettes,
walarekodi kesho yake” kelso alisema.
Kelso
anaishi Marekani tangu dec 27, 1979 na aliachana na muziki tangu enzi za Studio
One. Ingawa akirudisha nyuma kumbukumbu nzuri za familia yake ya The Wailers.zinazoishi,
anaona The Wailers ni taasisi bora ya muziki uliopendwa zaidi katika historia
ya muziki wa Jamaica.
Mwaka
2012 alisema anapanga kuandika kitabu kuhusu maisha yake na The Wailers.Kurudi
kwake na kuandika kitabu huenda isiwe karata ya mwisho ya Kelso,upande wa
muziki simmer down huenda ndiyo itakayomfanya akumbukwe kwayo.
Labda
sauti ya mwanzo ya vijana wadogo katika muziki maarufu ilisikika ikionya:
Chicken
merry, hawk de dear
and
when I’m de near you must be aware.
So
simmer down, Control your temper
Cause
the battle will be hotter
Nyimbo alizoshiriki
Simmer Down
The wailing wailers -1963
Ganja gun
I’m
still waiting
The
wailing waiters -1965
Rasta
Rude boy
The wailing wailers -1965
Ska
jerk
The
wailing wailers -1965
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni