Tafuta katika Blogu Hii

Ijumaa, 30 Oktoba 2015

Injili ya Barnaba



           Ni kitabu ambacho wakristo wengi hawajapata kukisikia au kukiona.
           Ni kitabu chenye sura 222, ambacho kilionekana kwa mara ya kwanza mwaka 1709 nchini Uholanzi, na mwaka 1738, Kilipelekwa Vienna Austria kwenye maktaba kuu ambako kimehifadhiwa mpaka leo.
          Kimeandikwa kwa lugha ya Kiitaliano sehemu za chini ya kurasa zake yameandikwa maneno kadha wa kadha kwa kiarabu.
Mwaka 1907 ilitolewa tafsiri ya kitabu kizima kwa lugha ya kiarabu kufuatia rai ya Seyyid Muhammad Rashid Ridha. Aliyetafsiri ni Dk Khalid sa’adah.
         Pia kimetafsiriwa katika lugha nyingine tofauti tofauti ikiwa pamoja na kiingereza.
         Upo utatanishi mkubwa kuhusu mtu aliyekiandika  kitabu hicho, upande ukidai mwandishi ni Barnaba yule kutoka Kipro (Cyprus) ambayo Luka aliandika habari zake akimwita Mtume, Nabii tena Mwalimu mtu mwema aliyejaa Roho Mtakatifu na imani (Matendo 14:4,14, 13:1 na 11:24). Inadaiwa kitabu hiki kiliibwa na mtawa mmoja aliyeitwa Fra Marino kutoka Vatican wakati wa Papa Sixtus (1589-1590) na kwamba awali kilitambulika kama injili harisi na kilitumika katika makanisa ya Alexandria hadi mwaka wa 325 baada ya Masihi. Kwa upande mwingine imeelezwa kwamba kwa vile katika sehemu zote zilizonukuu Torati katika kitabu hicho yametumiwa maneno yafananayo kabisa na yale yaliyotumika katika Biblia tafsiri ya Vulgata iliyoandikwa mwaka 380 baada ya Masihi, ni dhahiri mwandishi wake sio Barnaba. Pia umefanywa uchunguzi wa kisayansi juu ya karatasi ya mwandiko wa kitabu hicho na imethibitishwa kwamba kiliandikwa baada ya mwaka 1500. Inaaminika mwandishi wa kitabu hicho ni Mhispania mmoja aliyeitwa Mustafa.
         Tokea mwaka 1907 kilipotafsiriwa kitabu hicho katika lugha ya Kiarabu baadhi ya watu wamekuwa wakizungumzia na kudai kuwa kitabu hicho ndiyo inili pekee yake iliyo sahihi. Kukubaliwa na injili hiyo ya Barnaba bila shaka kunahusiana na kutajwa kwa Ismail katika sura ya 44 kuwa ndiye aliyekaribia katika kutolewa sadaka na babaye Ibrahimu, na siyo Isaka kama isemmavyo Biblia.
          Kivutio kingine katika kitabu hicho ni sura ya 212 inayoonesha Yesu akihofia kubadilishwa kwa injili, na sura ya 222 inayozungumzia watu iwaitao waovu walioeneza habari za kufa kwa Yesu Msalabani na kusema alikuwa mwana wa Mungu. Katika sura hiyo anatajwa Paulo kuwa ndiye aliyepotosha ukweli.
          Ubatili wa injili ya Barnaba unaonekana ndani ya kitabu hicho hicho kimehitilafiana sana na vitabu vilivyoandikwa na wanafunzi wa Yesu kama vile Mathayo, Yohana, Petro, Yakobo na Yuda. Imeeleza kwa mfano katika sura katika sura ya kwanza ya kitabu hicho kwamba Barnaba alikuwa mmoja wa wanafunzi wa Yesu. Lakini Barnaba ni mtu aliyefahamika kwa undani kwamba alikuwa binamu wa Marko, na kwamba aliingia katika ufuasi wa Yesu baada ya Pentecoste, ambayo ilikuwa ni siku ya hamsini baada ya kufufuka kwa Yesu. Barnaba hakuwa mwanafunzi wa Yesu. Hata jina la Barnaba alipewa na Petro na wenzake likiwa na maana ya “Mwana wa faraja” (Matendo 4:36, 37) Kabla ya hapo alifahamika kwa jina la Yusuph.
         Kuhitilafiana kwingine kwa injili ya Barnaba na vitabu vya Mathayo, Marko, Luka na Yohana ni katika maelezo ya sura ya 92, yesemayo Barnaba akiwa pamoja na Yesu waliamriwa na Malaika Mtakatifu waende kwenye mlima Sinai na kukaa huko siku arobaini.
Lakini inafahamika kwamba tokea alipowachagua wanafunzi wakae hadi alipopaa Yesu alikuwa ndani ya nchi ya Parestina tu, sio nje ya hapo (Mlima Sinai upo nchini Misri).
         Kutokufahamika huko kwa Jiografia ya Palestina na mwandishi wa kitabu cha injili  ya Barnaba kunajidhihilisha zaidi katika sura ya 20 inavyoeleza jinsi Barnaba alivyosafiri na Yesu katika mashua kwenye bahari ya Galilaya hadi kwenye mji wa Nazareti. Hili ni jambo lisilowezekana, Nazaleti iko  Kilometa zaidi ya 60 kuyoka bahari ya Galilaya. Pia katika sura ya 63 mji wa Ninawi ulioko Al Kishr kwenye mto wa Tigris umeelezewa kuwa ukingoni mwa bahari ya kati ( Mediteranea).
         Jambo linguine linalochanganya ni kuhusu majira. Sura ya 92:10 inaonyesha Yesu aliishi wakati mmoja na Muhammad, na kwamba Yesualifurahi alipomuona Muhammad akasema “ijapokuwa mimi sistahili kufungua gidamu za viatu (vya Muhammad), lakini nmepata rehema na rehema”. Pia ubatili wa injili ya Barnaba inajionysha sura ya 51:4-20  ambapo Mwenyezi Mungu ameelezewa jinsi alivyofanya maelewano mazuri kabisa na ibilisi.
          Ni wazi kabisa yeyote  asemaye injili ya Barnaba ndiyo sahihi hajasoma kitabu hicho.



Hakuna maoni: