Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 13 Desemba 2015

Rider Seventeeny

                                                         



Rider Seventeeny
Jina Peter Paschal Joseph
Kuzaliwa Arusha
Mwanamziki
Mtindo bongo flavor
Mwaka alioanza 2004
                    Alizaliwa hospitali ya Mount Meru iliyopo mkoani Arusha na kuanza masomo katika shule ya Msingi Kaloleni baada ya  mwaka mmoja wazaszi wake wakahamia Tanga ambako ni nyumba iliko mizizi ya ukoo wake. Hapo akaanza tena darasa la kwanza katika shule ya msingi St.Martin ambayo sasa inaitwa Magila wilayani Muheza  mkoani Tanga huo ulikuwa mwaka 2000.
Hakukaa sana Tanga baba yake alipata uhamisho wa kazi na kuelekea Dar  es salaam hapo hakuwa na hiari isipokuwa kukusanya virago vyake na kumfuata baba yake, kwa mara nyingine  tena akajikuta anaanza darasa la kwanza katika shule ya msingi Vingunguti A iliyopo wilaya ya Ilala huo ulikuwa mwaka 2001.
                            

 Kama kawaida ya vipaji vyote huanza kujitokeza umri mdogo akiwa shuleni akajikuta anapenda muziki na kutamani kuwa mwanamuziki mkubwa albam ya Dully sykes uluyokkwenda kwa jina la historia ya kweli  ilikuwa na wimbo uliobeba jina la historia ya kweli. Kulikuwa na wimbo uliobeba jina la Salome huo ndio uliompagawisha Rider kwa kiwango cha kutosha kumfanya aukariri mashairi yake pamoja na nyimbo zingine ikiemo Monalisa.
Taratibu alijifunza kuimba na kufunga nyimbo pamoja na kuigiza akishirikiana na baadhi ya wanafunzi wenzake waliokuwa  na vipawa vinavyofanana.
                   Mwaka 2004 walianzisha kundi waliloliita Son cost, Rider akiwa kiongozi akishirikiana na Yasco Taller pamoja na Bang'ala wa masoko.  Kundi liliendeshwa Kiugumu ugumu mpaka mwaka 2008  wlipofanikiwa kutoa wimbo ulioitwa Acha bifu waliorekodiwa  katika studio za Pamoja Records kwa Nas B na kinanda kama solo artist. Studio zilikuwa kinondoni mkwajuni hapa walitoa nyimba mbili.
Acha bifu ulionya wasanii wanajamii kuacha mivutano isiyo na tija wala maana yoyote nyimbo  hizo hazikufanikiwa kuchezwa redioni. Mwaka 2009 ulikuwa mwaka mgumu kwa kila manakundi. Wawili wliokuwa wana soma walijikita zaidi katika  masomo na mmoja alikuwa anafanyakazi na kukosa muda wa kufanya muziki kikamilifu. Hivyo kundi likafa kifo cha kawaida.
                            
Akiwa anasoma Secondary ya Msongola hakuacha sanaa imponyoke akageukia sanaa ya maigizo na kujikita katika uchezaji wa filam. Akafanikiwa kupata nafasi katika kundi la Alwatani Theatre Group lililo kuwa na maskani yake ilala likiongozwa na Haji Dilunga.
Akishiriki katika filamu ya Bunge la wachawi namba moja, Bunge la wachawi namba mbili, Popobawa na Zindiko alipopata nafasi ya kuingiza na Ahmed Ulotu (Mzee Chilo). Bada ya kumaliza kidato cha nne akarudi kwenye muziki. Akaanzisha kundi linaloitwa La Ukoo Entertainment.
Kundi lilianza kama masihara, sasa limekuwa kubwa likIshirikisha wasanii wa fani mbalimbali toka kona tofauti tofauti, wazo lilianzaia shuke utekelezapo wake ulipoanza hakukuwa na kusimama hata baada ya kumaliza shule wanebaki na La Ukoo Entertainment kundi likiwa na wachoraji, waigizaji Graphic Designers, vinyozi, wacheza mpira wote pamja wanaitwa La Ukoo. Si kwa maana ya watu wa asili ya sehemu moja la hasha isipokuwa Ukoo katika burudani ndipo wote wanajumuika chini ya  mwamvuli mmoja La Ukoo.
Kwa sapoti ya marafiki na La Ukoo akanza ktoa T-shirt zenye nemo ya la ukoo Entertainment. Milango iko wazi na kundi linapokea yeyote mwenye kipaji cha sanaa anayependa kujiunga 2012 alifanikiwa kutoa wimbo Nimedata akiwa amemshirikisha jay maswagger kutoka kundi la republic. Millionare lililokuwa chini ya  marehemu Sharo Millionere mwongozaji akiwa Dr. Babak na Big Josh imetengenezwa katika Studio za Kany  Records chini ya producer Man Lee” hii pia haijapata kuchezwa redioni ila inapatikana youtube kwa jina   rider 17 ft.Jay Maswagger
                                 
                    kama kawaida changamoto haikosekani popote hapa zinamkabili pia Rider kwenye kazi yake ameonyesha kipaji akabuni wazo , na kulifanyIa kazi lakini ukosefu  wa pesa ni changamoto kubwa na nzito kwake, kuikabili, pia msimamizi wa kazi zake pamoja na wadhamini bado hajawapata hivyo kumuwia vigumu kurekodi na kuzifanyia promo kazi zake zichezwe katika vituo vya radio na tv ziweze kuwafikia watu  kwenda Studio kwa miguu ni changamoto nyingine inayomkabili. Pia wapo watu wanaoshindwa kuthubutu kufanyia kazi mawazo yao. Hawa wanatumia midomo na nguvu zao kumkatisha tamaa ya kutimiza ndoto zake.Hivyo  yeyote mwenye kutaka kusukuma harakati hizi kwa michango ya hali na mali na mawazo mazuri milango iko wazi na anakaribishwa.Yote kwa yote hachoki anakaza mkwiji na kusonga mbele sasa anajiandaa kurekodi wimbo mpya na kutoa video yake wapenzi na mashabiki wake watapata kazi zake kupitia mitandao ya kijamii kueni mkao wa kula.

Hakuna maoni: