Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 6 Desemba 2015

Alvin “ Secco “ Patterson

Alvin Patterson


Alvin “ Secco “ Patterson
Jina kamili Fransisco Willie
Pia anajulllukana kama
 Alvin “ Secco “ Patterson,Secco Pep ,Willie Pep
Alizaliwa (1930-12-30)
Asili – Kingston Jamaica
Mtindo – Reggae
Mpigaji wa percurssion
Vyombo anavyopiga –percussion /bongo drum , conga, tambourine, cowbell, nk.
Mwaka aliofanya kazi 1969 mpaka sasa
Alioshirikiana nao
Bob Marley & The Wailers,The Wailers
Alvin “ Secco “ Patterson
             Alizaliwa tarehe 30 Desemba 1930, Havana (Cuba) ni mpiga percussion alikuwa mwanakundi wa The Wailers band
Alvin  alikuwa ni mpiga percussion katika Bob Marley and The Wailers na ni mmoja kati ya marafiki wa karibu sana wa Bob Marley. Ingawa anajulikana kama “Secco”alizaliwa akaitwa Fransisco Willie, Havana Cuba na baba mwenye asili ya Jamaica na mama Mpanama akiitwa Cellestina Hardin. Alichagua jina la Alvin Patterson kama jina la kisanaa na alipata jina la “Secco” kama kifupisho cha jina lake la Fransisco alihamia Jamaica na wazazi wake waliishi Westmorland, ambako wazazi wake walikuwa wanajishughulisha na kilimo baadaye akahamia Kingston na mama yake baada ya wazazi wake kuachana, kama kijana Patterson alitafuta kazi katika mgodi wa madini ya bauxite
              Mwaka 1957 Patterson aliamua kuhamia Marekani kutafuta kazi yenye kipato zaidi. Akiwa katika safari yake ajali mbaya ilitokea ya treni ilitokea 1st September.   Mara moja Patterson alirudi kisiwani kuwatafuta ndugu zake aliohofia wanaweza kuwemo kati ya watu 200 waliofariki au 700 waliojeruhiwa. Na wazo lake la kuondoka likafutika ma akarudi jumla Kingston katika mgodi wa bauxite.
              Ilikuwa kipindi hiki ndipo Patterson kwa mara ya kwanza alipo kutana na Bob Marley  akiwa na miaka kumi na tano, mdogo kwa Patterson tofauti ya miaka kumi na tano na waliishi wote  eneo moja katika makazi  duni ya  watu masikini Trech town. Marley alimwona Patterson sababu ya umaarufu wake wa mchezo wa cricket, alikuwa na uwezo mkubwa wa kuucheza na akaanza kumfuatilia Patterson mara kwa mara, akitafuta ujuzi wa criket na pia akivutiwa na muonekano wa Alvin Patterson
Wakazama katika urafiki na Marley na wakabaki hivyo mpaka mwisho wa maisha ya Marley. Patterson alimtia moyo Marley  wakati anaanza kujaribu kuimba muziki,akiwa Patterson mwenyewe alipata uzoefu katika muziki wa kupiga percussion kwa mwanamuziki maarufu wa Calypso akiitwa Lord Flea na wapiaji wengine  namna ya kupiga combo za kikalypso. Na alikuwa ni Patterson kwanza aliyelichukua kundi la The Wailers. Likiwahusisha Marley, pamoja na Peter Tosh na Bunny Wailer kulipeleka studio za Coxsson  dodd kwa mara yao ya kwanza july 1963.  Makubaliano yalifikiwa na The Wailers  wakatoa muziki uliotikisa “simmer down” wimbo uliomtambulisha Marley
                    Wakati wailers ikijitanua katika muziki Jamaica,Patterson aliendelea kifanyakazi katika mgodi wa bauxite, mwaka 1966 wakati Marley akifanyakazi Marekani, Patterson alijeruhiwa katika ajali iliyotokea katika mgodi, wakati bomba la gasi iliyopita chini ya sakafu ya canteen ilipopasuka, ikasababisha mlipuko ulioacha wafanyakazi wengi kujeruhiwa vibaya. Patterson alitupwa nje ya jengo na akapoteza viatu katika tukio hilo wakati  Marley aliporudi kisiwani wiki kadhaa baadaye , alimshawishi Patterson  kuachana na kazi ya mgodini na aanze kujikita katika muziki matokeo yake Patterson akaanza kuchangia percussion katika nyimbo zilizofuata za The Wailers mchango wake wa kwanza unaojuikana ulikuwa juni 1967walipotoa “ lyrical satirycal” na this train” ziliachiwa na the wailers zikihusisha wail n soul M label. Wakati ushiriki wa Patterson katika Original Wailers (ikiwahusisha Tosh na Bunny) ulikuwa mdogo, lakini mchango wake ulizidi kuongezrka. Wakati Original Wailers walipokwenda  ziara yao ya kwanza (pekee)uingereza  mwaka 1973. Patterson alishiriki kama mtu wa kipekee kwenye ubunifu wa kiasili(root)
                   Wakati ushirikiano wa Marley, Tosh na Bunny ulipoisha Paterson akawa kiini cha kuihuisha bendi upya kwa maelezo ya Marley na akashiriki kila rekodi na  maonesho yote ya jukwaani ambayo Marley alifanya kwa maisha yake yote, Patterson akazama katika muziki na rekodi walizofanya  akibuni na kufanya muziki   uonekane wa kiasili.
Chupa ya maziwa katika “jamming” na muitikio wake sauti ya percussion katika “crazy baldhead” ni miongoni mwa mifano bora kabisa ya mitindo yake ya kufanya. Kitu rahisi kwa ubora wa juu. Ingawa hakutajwa Patterson anaaminika aliandika baadhi ya nyimbo za marley ukijumlisha na “work”.
                     
Wakati wote wa maisha ya marlley Patterson alikuwa karibu yake. Mwaka 1976,Patterson alikuwa anafanya mazoezi na Marley akiwa barabara ya 56 Hope (road) ambapo mtu mwenye bunduki alimjeruhi Marley, pia walikuwepo mkewe Marley na meneja Don Taylor. Septemba 1980 Patterson alikuwa na Marley wakati alipopatwa shambulio la ugonjwa  wakati anafanya mazoezi ya mbio (jigging) centra park na akabaki na Marley wakati  wote wa matibabu yake ya kansa new York, marekani mpaka katika kliniki ya Dr Jose Issels.
Rottach-Egern, Ujerumani.
Kufuatia kifo cha Marley, Patterson aliendelea music na The Wailers band . mwaka 1990 Patterson alipata shambulio la ubongo, (haemorrhage) akiwa ziarani Brazil shambulio lililokaribia kupoteza maisha yake alipopata nafuu akaachana na muziki wa jukwaani isipokuwa anaonekana tu katika matamasha mbalimbali yanayomuhusisha Marley . Patterson sasa anaishi kingston.

Hakuna maoni: