Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 13 Septemba 2015

SHEIKH ZUBEIR BIN ALLY MUFTI MPYA TANZANIA



     
 
Sheikh mkuu,mufti wa Tanzania Abubakar Zubeir bin Ally
      Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA) limemchagua sheikh Abubakar Zubeir bin Ally kuwa mufti wa Tanzania, kwenye  mkutano mkuu wa uchaguzi uliofanyika mjini Dodoma.
       Uchaguzi huo umefanyika baada ya kifo cha aliyekuwa mufti wa Tanzania. Sheikh Issa bin Shaaban Simba aliyefariki juni 15 mwaka huu kwenye hospitali ya TMJ jijini Dar es salaam,kwa ugonjwa wa kisukari na presha.
       Sheikh Abubakar Zubeir alichaguliwa baada ya kuwashinda masheikh wengine watatu waliojitokeza kushindania nafasi hiyo.
       Mwanazuoni huyo ndiye aliyekaimu wadhifa huo kwa miezi mitatu baada ya kifo cha mufti Simba, alichaguliwa kwenye mkutano wa dharura uliojumuisha wadhamini wa baraza hilo, maulamaa, masheikh wenyeviti wa mikoa na wilaya waliojumuika katika ukumbi wa hotel ya African dreams uliopo area D mjini Dodoma.
     
  Sheikh Zubeir alishinda baada ya jina la sheikh Hassan Kiburwa kutoka Kigoma kukatwa kwa kutokidhi viwango sheikh Mtupa na sheikh Ally Muhidini Mkoyagane kujitoa kwa hiari yao katika mpambano huo hivyo sheikh Abubakar Zubeir kupita bila kupingwa katika mkutano uliohudhuriwa na wajumbe wa Bakwata zaidi ya mia tatu,na kuendelea kuandika historia.
       Katika hotuba yake ya shukrani, Sheikh mkuu, mufti Abubakar alishukuru kamati ya  Bakwata pamoja na wajumbe wote wa mkutano huo, alisema atafanya kazi yake kwa uandilifu na kuwaunganisha waislamu ambao wanaonekana kukata tamaa katika nchi yao wenyewe.
       “Nawashukuru kwa ushirikiano mlioniomnyesha na nInaahidi kuyasimamia yote mliyoyasema wakati nilipokaimishwa nafazi hii kule Bagamoyo na kubwa kufanyakazi na taasisi zote za dini zilizopo hapa nchini na nje ya nchi kwa mslahi ya waislam.Lakini pia niliahidi huko nyuma juu ya kuifanyia marekebisho katiba yetu ya Bakwata namuomba Mwenyezi MUNGU aniwezeshe nianikishe hilo kwa faida ya waislam wote na yeyote mwenye mawazo mema kw ajili ya kuboresha hali ya waislam nchini,milango iko wazi  namkaribisha kwa ushauri mzuri” alisema mufti. Aliwaomba waislam wote nchini kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu wa octoba 25 mwaka huu na kumtaka kila mmoja kumchagua kiongozi atakayeona anamfaa kwa ajili ya maendeleo ya eneo lake na taifa kwa ujumla.
        
Sheikh mkuu huyo amekuwa ndani ya Bakwata,akiwa mjumbe wa baraza la ulamaa tangu wakati wa uongozi wa mufti Hemed hin Jumaa bin Hemed.
Alikuwa naibu mufti wa Tanzania katika kipindii cha uongozi wa sheikh mkuu isa bin Shabani Simba na baadaye kuwa naibu kadhi nkuu wa Tanzania baada ya cheo cha unaibu mifti kufutwa kwenye katiba ya bakwata.
         Sheikh Abubakar ni zao la masheikh wakubwa nchini kama akina sheikh Hassani hin Ameer aliyeupokea uhuru wa Tanganyika mwka 1961,uwanja wa taifa Dar es Salaam,sheikh Abdallah Farsy wa Mombasa, sheikh Mohamed Ramia wa Bagamoyo sheikh Mohamed bin Ayoub wa Tanga, mufti sheikh mkuu Hemed bin Jumaa bin Hemed.


         Na kuahidini kuwa nitafanya wema, uadilifu na heshima ya nchi yetu ili wote tumwabudu Allah (S.W) kwa amani na usalama “alisema mufti wa  Jamuhuri ya muungano wa Tanzania sheikh abubakar zubeir bin ally.


Hakuna maoni: