Tafuta katika Blogu Hii
Ijumaa, 18 Machi 2016
Korea Kaskazini yajaribu makombora
Korea Kaskazini imefyatua makombora mawili ya masafa ya kati, siku
chache tu baada ya kiongozi wake Kim Jong-Un kuahidi kufanya majaribio
kadhaa ya silaha za nyuklia na makombora, wakati ambapo mvutano wa
kijeshi ukizidi. Msuguano kati ya Korea mbili zilizogawika umeongezeka
tangu Korea Kaskazini ilipofanya jaribio lake la nne la nyuklia Januari
6, na kufuatiwa mwezi mmoja baadaye na ufyatuaji wa roketi ambao
ulichukuliwa na wengi kama kificho cha jaribio la kombora la masafa
marefu. Maafisa wa Marekani wamesema walifuatilia ufyatuaji wa makombora
mawili ya Rodong -- yanayoaminika kuwa ya masafa ya kati kutokea kwenye
magari. Kombora la Rodong lina uwezo wa kwenda umbali wa kilomita
1,300.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni