Tafuta katika Blogu Hii

Jumatatu, 28 Septemba 2015

Viongozi wa Burkina Faso walioshikiliwa wapo salama

Brigedia jenerali Gilbert Diendéré wa Burkina FasoMkuu wa baraza jipya la utawala Burkina Faso alisema Rais na Waziri Mkuu wapo salama chini ya ulinzi wa jeshi na karibuni wataachiwa.
Brigedia Jenerali, Gilbert Diendere alizungumza na Sauti ya Amerika hapo Alhamis, siku moja baada ya wanajeshi kuiangusha serikali ya muda kwenye taifa la Afrika magharibi na kuwakamata viongozi wake. Jenerali huyo alisema jeshi lilipanga mapinduzi kwa sababu utaratibu wa kisiasa nchini humo haukuwa wa haki.
Alisema ataanza mashauriano ya kisiasa yanayojumuisha pande zote. Burkina Faso ilipanga kufanya uchaguzi wa urais na bunge hapo Oktoba 11. Tarehe hiyo hivi sasa ipo njia panda.
Waandamanaji vijana wa Burkina faso
Waandamanaji vijana wa Burkina faso
Watu wasiopungua watatu waliripotiwa kuuwawa wakati waandamanaji vijana walipojaribu kukusanyika karibu na makazi ya rais huko Ouagadougou na ubalozi wa Marekani ulisema vizuizi vya barabarani vimewekwa kote mjini humo.
White House mjini Washington ililaani vikali kile ilichokiita jaribio ambalo ni kinyume cha katiba la kuchukua madaraka. Naibu msaidizi wa Umoja wa Afrika, Erastus Mwencha aliwataka Alhamis viongozi hao wa kijeshi haraka kukabidhi madaraka kwa serikali ya muda. “Serikali yeyote ambayo haifuati katiba inalaumiwa moja kwa moja kwa sababu tunaamini katika utawala wa sheria na mabadiliko yeyote ya madaraka lazima yafuate utaratibu wa katiba”, alisema Mwencha.
Pia aliwasihi watu kutoshirikiana na jeshi kuchukua madaraka.
Serikali ya muda ilichukua madaraka nchini Burkina Faso wakati ghasia maarufu zilizomuondoa Rais Blaise Compaore madarakani mwezi Oktoba mwaka jana baada ya kuwepo mamlakani kwa miaka 27. Alipanga kubadili katiba ili aweze kuongeza utawala wake.

Jumapili, 27 Septemba 2015

Mkuu wa baraza jipya la utawala Burkina Faso alisema Rais na Waziri Mkuu wapo salama chini ya ulinzi wa jeshi na karibuni wataachiwa.

Mkuu wa baraza jipya la utawala Burkina Faso alisema Rais na Waziri Mkuu wapo salama chini ya ulinzi wa jeshi na karibuni wataachiwa.
Brigedia Jenerali, Gilbert Diendere alizungumza na Sauti ya Amerika hapo Alhamis, siku moja baada ya wanajeshi kuiangusha serikali ya muda kwenye taifa la Afrika magharibi na kuwakamata viongozi wake. Jenerali huyo alisema jeshi lilipanga mapinduzi kwa sababu utaratibu wa kisiasa nchini humo haukuwa wa haki.
Alisema ataanza mashauriano ya kisiasa yanayojumuisha pande zote. Burkina Faso ilipanga kufanya uchaguzi wa urais na bunge hapo Oktoba 11. Tarehe hiyo hivi sasa ipo njia panda.
Waandamanaji vijana wa Burkina faso
Waandamanaji vijana wa Burkina faso
Watu wasiopungua watatu waliripotiwa kuuwawa wakati waandamanaji vijana walipojaribu kukusanyika karibu na makazi ya rais huko Ouagadougou na ubalozi wa Marekani ulisema vizuizi vya barabarani vimewekwa kote mjini humo.
White House mjini Washington ililaani vikali kile ilichokiita jaribio ambalo ni kinyume cha katiba la kuchukua madaraka. Naibu msaidizi wa Umoja wa Afrika, Erastus Mwencha aliwataka Alhamis viongozi hao wa kijeshi haraka kukabidhi madaraka kwa serikali ya muda. “Serikali yeyote ambayo haifuati katiba inalaumiwa moja kwa moja kwa sababu tunaamini katika utawala wa sheria na mabadiliko yeyote ya madaraka lazima yafuate utaratibu wa katiba”, alisema Mwencha.
Pia aliwasihi watu kutoshirikiana na jeshi kuchukua madaraka.
Serikali ya muda ilichukua madaraka nchini Burkina Faso wakati ghasia maarufu zilizomuondoa Rais Blaise Compaore madarakani mwezi Oktoba mwaka jana baada ya kuwepo mamlakani kwa miaka 27. Alipanga kubadili katiba ili aweze kuongeza utawala wake.

Jumatatu, 21 Septemba 2015

Kuzidi hofu ya madhara ya jinai za Saudia nchini Yemen

  Wasiwasi wa taasisi za kimataifa na za nchini Yemen kuhusu jinai za ukoo wa Aal Saud nchini humo umeongezeka mno hivi sasa huku Saudia na kundi lake la nchi zinazotenda jinai, zikizidisha ukatili wao dhidi ya wananchi wasio na ulinzi wa Yemen. Jeremy Hopkins, mjumbe wa Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF nchini Yemen ametoa tamko kuhusu kuongezeka jinai na uvunjaji wa haki za wananchi wa Yemen na kuharibiwa miundombinu ya nchi hiyo maskini ya Kiarabu, na kusema kuwa, ana wasiwasi mkubwa wa kutofika shehena ya misaada ya kibinadamu kwa watu 11 elfu waliokwama huko kusini mwa mji mkuu wa Sana’a, kutokana na mashambulizi ya kikatili ya Saudia. Jeremy Hopkins ameongeza kuwa, kitendo cha wanajeshi wa Saudia cha kushambulia shehena za misaada ya kibinadamu na maeneo ya kusafishia maji nchini Yemen kinasikitisha sana na kimewasababishia matatizo makubwa wakazi wa eneo hilo. Wizara ya Afya ya Yemen jana Jumamosi ilitoa taarifa na kusema kuwa hospitali za mji mkuu Sana’a hazina uwezo tena wa kupokea majeruhi na zimekumbwa na uhaba mkubwa wa madawa, mafuta na mahitaji mengine ya lazima. Wizara ya Afya ya Yemen imezitaka taasisi za kimataifa kuchukua hatua za haraka za kuwaokoa wagonjwa na majeruhi wa mashambulio ya anga ya Saudia. Muhammad al Masouri, Katibu Mkuu wa taasisi ya masuala ya kisheria ya “al Bayt al Qanuni” ya Yemen amesema kuwa, hivi sasa haiyumkiniki tena kuzalisha maji safi nchini humo kutokana na kukatika umeme na kuharibiwa mabomba ya mafuta. Ametahadharisha kuwa, wananchi milioni 27 wa Yemen wanakabiliwa na hatari kutoka kila upande. Wanajeshi wa utawala wa ukoo wa Aal Saud jana Jumamosi pia waliendelea kufanya jinai kwenye maeneo ya makazi ya raia katika mikoa ya Sana’a, Sa’ada, Taez, al Baydha na al Hudaydah nchini Yemen na kuua makumi ya wananchi wasio na hatia kujeruhi wengine 100. Vile vile ndege vamizi za Saudia na genge lake zimeshambulia mara 20 majengo ya Wizara ya Vijana, Wizara ya Mambo ya Ndani na kituo cha polisi huko Sana’a. Amma cha kusikitisha zaidi ni kuona kuwa jinai hizo za Saudi Arabia zinafanyika mbele ya macho ya jamii ya kimataifa na mashirika yanayojigamba kuwa ni watetezi wa haki za binadamu na utawala wa sheria, ulimwenguni. Kimya cha mashirika hayo kimezidi kuwa kikubwa katika hali ambayo, shirika la habari la al Ahd la nchini Yemen limeripoti kuwa, Saudi Arabia inatumia pia makombora yenye gesi ya sumu dhidi ya wananchi wa Yemen. Kwa mujibu wa shirika hilo, gesi hizo za sumu zilizoenea kwenye makazi ya raia na mashamba ya kilimo, zimepelekea kuzuka magonjwa ya ajabu nchini Yemen. Houthis 

Sudan yatoa wito dhidi ya Israel

Sudan yatoa wito wa kusimama kidete dhidi ya Israel
Serikali ya Sudan imeutaka ulimwengu wa Kiarabu na Kiislamu kusimama kidete mkabala na jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Masjidul Aqswa. Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Sudan imetoa taarifa kuhusiana na uvamizi na hujuma za Israel na mashambulio ya walowezi wa Kizayuni dhidi ya Masjidul Aqswa na waumini wa Kipalestina wanaotekeleza ibada katika msikiti huo na kuonyesha kuchukizwa mno na hatua hizo za Wazayuni. Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Sudan  imeutaka ulimwengu wa Kiarabu na Kiislamu kuitisha mkutano wa dharura kwa ajili ya kutafuta njia za lazima za kukabiliana na jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel katika msikiti wa al-Aqswa na kusimama kidete mkabala na jinai hizo za kinyama. Taarifa hiyo ya Wizara ya Mashauri ya Kigeni wa Sudan imebainisha kwamba, kusimama kidete na kuweko umoja katika ulimwengu wa Kiarabu na Kiislamu ni jambo la lazima kwa ajili ya kuhitimisha uvamizi na hujuma za Israel na kuzuia kubomolewa msikiti huo mtakatifu. Masjidul Aqswa ni eneo la tatu kwa utukufu kwa Waislamu baada ya Masjidul Haram mjini Makka na Masjidun Nabawi mjini Madina huko Saudi Arabia. Katika miaka ya hivi karibuni, Israel imeshadidisha njama na hujuma zake dhidi ya eneo hilo takatifu.

Jumapili, 13 Septemba 2015

SHEIKH ZUBEIR BIN ALLY MUFTI MPYA TANZANIA



     
 
Sheikh mkuu,mufti wa Tanzania Abubakar Zubeir bin Ally
      Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA) limemchagua sheikh Abubakar Zubeir bin Ally kuwa mufti wa Tanzania, kwenye  mkutano mkuu wa uchaguzi uliofanyika mjini Dodoma.
       Uchaguzi huo umefanyika baada ya kifo cha aliyekuwa mufti wa Tanzania. Sheikh Issa bin Shaaban Simba aliyefariki juni 15 mwaka huu kwenye hospitali ya TMJ jijini Dar es salaam,kwa ugonjwa wa kisukari na presha.
       Sheikh Abubakar Zubeir alichaguliwa baada ya kuwashinda masheikh wengine watatu waliojitokeza kushindania nafasi hiyo.
       Mwanazuoni huyo ndiye aliyekaimu wadhifa huo kwa miezi mitatu baada ya kifo cha mufti Simba, alichaguliwa kwenye mkutano wa dharura uliojumuisha wadhamini wa baraza hilo, maulamaa, masheikh wenyeviti wa mikoa na wilaya waliojumuika katika ukumbi wa hotel ya African dreams uliopo area D mjini Dodoma.
     
  Sheikh Zubeir alishinda baada ya jina la sheikh Hassan Kiburwa kutoka Kigoma kukatwa kwa kutokidhi viwango sheikh Mtupa na sheikh Ally Muhidini Mkoyagane kujitoa kwa hiari yao katika mpambano huo hivyo sheikh Abubakar Zubeir kupita bila kupingwa katika mkutano uliohudhuriwa na wajumbe wa Bakwata zaidi ya mia tatu,na kuendelea kuandika historia.
       Katika hotuba yake ya shukrani, Sheikh mkuu, mufti Abubakar alishukuru kamati ya  Bakwata pamoja na wajumbe wote wa mkutano huo, alisema atafanya kazi yake kwa uandilifu na kuwaunganisha waislamu ambao wanaonekana kukata tamaa katika nchi yao wenyewe.
       “Nawashukuru kwa ushirikiano mlioniomnyesha na nInaahidi kuyasimamia yote mliyoyasema wakati nilipokaimishwa nafazi hii kule Bagamoyo na kubwa kufanyakazi na taasisi zote za dini zilizopo hapa nchini na nje ya nchi kwa mslahi ya waislam.Lakini pia niliahidi huko nyuma juu ya kuifanyia marekebisho katiba yetu ya Bakwata namuomba Mwenyezi MUNGU aniwezeshe nianikishe hilo kwa faida ya waislam wote na yeyote mwenye mawazo mema kw ajili ya kuboresha hali ya waislam nchini,milango iko wazi  namkaribisha kwa ushauri mzuri” alisema mufti. Aliwaomba waislam wote nchini kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu wa octoba 25 mwaka huu na kumtaka kila mmoja kumchagua kiongozi atakayeona anamfaa kwa ajili ya maendeleo ya eneo lake na taifa kwa ujumla.
        
Sheikh mkuu huyo amekuwa ndani ya Bakwata,akiwa mjumbe wa baraza la ulamaa tangu wakati wa uongozi wa mufti Hemed hin Jumaa bin Hemed.
Alikuwa naibu mufti wa Tanzania katika kipindii cha uongozi wa sheikh mkuu isa bin Shabani Simba na baadaye kuwa naibu kadhi nkuu wa Tanzania baada ya cheo cha unaibu mifti kufutwa kwenye katiba ya bakwata.
         Sheikh Abubakar ni zao la masheikh wakubwa nchini kama akina sheikh Hassani hin Ameer aliyeupokea uhuru wa Tanganyika mwka 1961,uwanja wa taifa Dar es Salaam,sheikh Abdallah Farsy wa Mombasa, sheikh Mohamed Ramia wa Bagamoyo sheikh Mohamed bin Ayoub wa Tanga, mufti sheikh mkuu Hemed bin Jumaa bin Hemed.


         Na kuahidini kuwa nitafanya wema, uadilifu na heshima ya nchi yetu ili wote tumwabudu Allah (S.W) kwa amani na usalama “alisema mufti wa  Jamuhuri ya muungano wa Tanzania sheikh abubakar zubeir bin ally.


Jumatano, 9 Septemba 2015

Polisi wazuia shambulizi la kigaidi-Kenya

           Polisi nchini Kenya Jumanne waliwakamata watu watatu waliogundulika wakiwa na bomu la kienyeji walipoingia kwenye eneo la maduka ya kifahari.Kwa mujibu wa idara ya polisi ya Kenya bomu hilo liliteguliwa kwa usalama  na kulidhibiti lisilipuke.
           Mkuu wa polisi, bwana Robinson Mboloi  ambaye anaongoza kituo cha polisi cha Kasarani katika mji mkuu Nairobi akisema kuwa wamewatia mbaroni wanaume watatu ambao waligundulika kuwa na bomu hilo la kienyeji na kitufe cha kulilipua.  Eneo la maduka ambalo wanaume hao walikamatwa ni la Garden City Mall.    
           Bwana Mboloi alisema maafisa wa kitengo kinachoshughulika na milipuko walitegua bomu hilo  na eneo hilo la maduka liko salama.
Eneo hilo la maduka ambalo liko mjini Nairobi lilifunguliwa mapema mwaka huu, na kuelezewa kuwa kituo kikubwa cha maduka ya kifahari katika Afrika mashariki.
Kenya imekumbwa na mlolongo wa mashambulizi yaliyofanywa na waasi wenye uhusiano na kundi la wanamgambo wa kisomali la Al-shabaab ambao miaka miwili iliyopita walishambulia eneo la maduka la kifahari la Westgate Mall.
         Katika shambulizi hilo wanamgambo hao wa kiislamu walivamia na kuua watu takriban 67 na wafanyakazi katika siku nne za ghasia  wakidai ni majibu kwa jeshi la Kenya kuwepo nchini Somalia.
Wanaume watatu waliokamatwa Jumanne wameripotiwa  kuwa wote ni wakenya na walisimamishwa wakiwa pamoja na maafisa usalama kwenye eneo la ukaguzi la kuingia  kwenye kituo cha maduka.
Mboloi alisema kitufe cha kutegua bomu kilionekana wakati wa ukaguzi na shukran kwa kazi nzuri ya wana usalama.  Na kuongezea watachunguzwa  ili kufahamu mahusiano yao na ugaidi wa kundi la Al-shabaab.
Tangu mashambulizi ya Westgate, kundi la Al-shabaab limeendelea kuishambulia Kenya ndani ya ardhi yake huku shambulizi kubwa zaidi likiwa ni lile la mwezi April  mwaka huu wakati washambuliaji wanne wa kujitoa mhanga walipowaua watu 148 katika chuo kikuu cha Garissa kilichopo kaskazini mashariki mwa Kenya, wengi wao wakiwa wanafunzi.

PAPA KURAHISISHA SHERIA YA TALAKA

Papa Francis anatarajia kurahisisha taratibu zinazoruhusu wafuasi wa kanisa katoliki waliooana kutoa talaka na kuolewa tena huku wakibakia kuwa wafuasi wa katika kanisa hilo .
Maelezo ya taratibu hizo yanatarajiwa kutangazwa mjini Vatcan baadaye leo .
Papa aliunda tume ya wanasheria wa kanisa mwaka jana kupiga msasa mbinu ya kurekebisha taratibu hizo zinazoruhusu wanandoa kuachana na kupunguza gharama .
Bila sheria hiyo wanandoa wa kikatoliki wanaotalikiana na kuolewa upya hutazamwa kama wazinifu na hawaruhusiwi kupokea komunio.
 Papa Francis hatabadilisha mafunzo ya katoliki kuhusu kuachana kwa wanandoa , lakini atawezesha kurahisisha wanandoa wenye matatizo kuthibitisha kuwa ndoa yao haikuwa ya maana tangu mwanzo

Jumatano, 2 Septemba 2015

Hotuba ya Dr. Slaa kwa vyombo vya habari Serena Hotel Sept 1.

1.Napenda  kumshukuru  mwenyezi  mungu  kwa  kutujalia  uzima.


2. Nimeamua  kujitokeza  leo  hii  ili  kukomesha  upotoshaji  na  kuuweka  wazi  ukweli.



3.Sina  tabia  ya  kuyumbishwa  na  ninasimamia  ninachokiamini.


4.Sina  ugomvi  na  kiongozi  yeyote  maana  siasa  sio  uadui.


5. Siasa  inapoongozwa  kwa  misingi  ya  upotoshaji, matokeo  yake  ni  vurugu.


6. Naweka  wazi  kuwa  mimi  sikuwa  likizo  na  hakuna  mtu  yoyote  aliyenipa  likizo.


7.Kilichotokea  ni  kuwa  niliamua  kuachana  na  siasa  tangu  tarehe  28.7.2015  saa  sita  usiku  baada  ya  kutoridhishwa  na  kilichokuwa  kinaendelea  ndani  ya  chama  changu.


8.Ni  kweli  nilishiriki  kumleta  Lowassa  CHADEMA  Lakini  nilikuwa  na  misimamo  yangu  ambayo  ilitufanya  tusielewane.


9. Baada  ya  Lowassa  kukatwa  pale  Dodoma, Gwajima  ambaye  ni  mshenga  wa  Lowassa  alinipigia  simu  kutaka  kujua  ninii  cha  kufanya.


10. Nilimpigia   Mwenyekiti    Mbowe  kumjulisha  na  tukakubaliana  kupanga  muda  wa  kuwasikiliza.


11. Kabla  ya  kuanza  kuwasikiliza, msimamo  wangu  ulikuwa  ni  kumtaka  Lowassa  kwanza  atangaze  kuhama  chama, aweke  wazi  ni  chama  gani  anaenda  na  ajisafishe  juu  ya  tuhuma  zake

12.Tangu  akatwe  jina, Lowassa  hakutangaza  kujitoa  CCM  na  wala  hakujisafisha  na  tuhuma  zake, kitu  kilichonifanya  nitofautiane  naye.

13. Niliwauliza  wanachadema  wenzangu  kuwa  Lowassa  anakuja  kama  Mtaji  au  Mzigo?

14. Swala  sio  urais  kama  watu  wanavyozusha, mimi  nilikuwa  nataka  mgombea  mwenye  uwezo  na  sifa  ambaye  ataweza  kuitoa  CCM.  Sikuwa  na  tamaa  ya  urais  kama  watu  wanavyosema

15. Tangu  Gwajima  atupe  taarifa  za  ujio  wa  Lowassa, Swali  langu  la  Lowassa  kuwa  Mtaji  au  mzigo  halikuwahi  kujibiwa.

16. Nilitaka  kujua  ni  mtaji  gani  lowassa  atakuja  nao  na  ni  viongozi  gan  atakuja  nao.

17. Nilijibiwa  kuwa  anakuja  na  wabunge  50  wa  CCM, wenyeviti  22  wa  mikoa  na  wenyeviti  80  wa  wilaya.

18.Baada  ya  ahadi  hiyo, nilitaka  sasa  nipewe  majina  ya  hawa  watu  lakini  mpaka  tarehe  25  july  sikupewa  hayo  majina

19. Wenzangu  waliniambia  kuwa  tarehe  27  niitishe  kikao  cha  dharura  ila  niligoma  kwa  sababu  nilikuwa  sijapewa  haya  majina

20. Ndani  ya  kikao  hicho,  tulianza  kwa  mabishano  makali  kati  yangu  na  Mbowe, Lissu  na  Gwajima, viongozi  wenzangu  ni  shahidi  na  mungu  anajua. Msimamo  wangu  ulikuwa  ni  uleule  kujua  mchango  wa  Lowassa

21. Kikao  kile  kikavunjika, baadae  tukaingia  kamati  kuu  lakini  bado  msimamo  wangu  ulikuwa  ni  uleule. Baadae  nikaandika  barua  ya  kujiuzulu.

22.Profesa  Safari  aliichana  ile  barua.

23.Cha  kusikitisha  ni  kuwa  Kesho  yake  picha  zikaanza  kusambaa  mtandaoni  zikimuonyesha  na  lowassa  japo  viongozi  wangu  walizikana  zile  picha.  Kibaya  ni  kuwa  viongozi  waliuficha  ukweli

24.  Kesho  yake  niliandika  tena  barua  rasmi  ya  kujiuzulu.

25. Baada  ya  pale  zikaanza  propaganda  za  uongo  zikimuhusisha  hadi  mke  wangu  eti  kanizuia.

26. Naomba  watanzania  wajue  kuwa  mke  wangu  hakuwahi  kunizuia  kwa  lolote, lkn  hata  angefanya  hivyo  sio  mbaya  maana  hata  yeye  ni  mwanaharakati  mwenye  uchungu  na  nchi  hii.

27. Mke  wangu  aliwahi  hadi  kuumia  wakati  akipigania  ukombozi  wa  nchi  hii.....Lakini  sio  mbaya, familia  yangu  imezoea  propaganda.

28. Kikubwa  katika  harakati  ni  credibility  ambayo  lazima  uilinde  na  mimi  sitaki  jina  langu  liharibiwe  na  ni  haki  yangu.

29. Maslah  mapana  ya  taifa  ndiyo  yaliyotufikisha  hapa  na  sio  maslahi  binafsi.

30.Lowassa  na  wapambe  wake  ni  waongo  maana  hakuna  hata  kipengele  kimoja  walichokitekeleza.

31. Tulitaka  hao  wabunge  50  waje  kwanza  kabla  ya  mchakato  wa  uteuzi  ccm

32. Napinga  kuchukua  makapi  ya  CCM  na  kuyaita  MTAJI.

33.Mtu  kama  Sumaye  ni  FISADI  na  nilikuwa  siongei  naye

34. Sumaye  aliwahi  kusema  CCM  wakimchagua  Lowassa  atahama  chama. Leo  Lowassa  kawaje  msafi??

35. Tulitaka  Mtaji  toka  kwa  Lowassa  na  sio  MAKAPI

36. Wenyeviti  walioletwa  na  Lowassa  ni  MIZIGO  na  namjua  vizuri. Akithubutu  kunijibu  ntamwaga  UOZO  wake  wote

37.Nani  asiyejua  Guninita  pia  ni  mzigo??

38:  Nawataka  viongozi  wangu  wanijibu  ni  mtaji  upi  walioupata  toka  kwa  Lowassa.

39. Mimi  ni  Padri  Mstaafu, sipendi  siasa  za  uongo.

39. Ukisema  unataka  kuiondoa  CCM  ni  lazima  ujikumbushe  misingi  ya  CHADEMA  ambayo  ilikuwa  ni  uadilifu. Leo  chadema  hii  ina  Uadilifu  gani??

40.  Namshangaa  sana  Lowassa  eti  kusimama  mbele  ya  watu  akijinasibu  kuwa  ni  msafi.....kwamba  mwenye  ushahidi  aende  Mahakamani. Ni  dhambi  kupotosha  watu.

41. CCM    hawana  ujasiri, ni  waoga  na  ndiyo  maana  wamewalea  watu  kama  akina  Lowassa

42. Ukitoa  kinyesi  chooni  na  kukipeleka  Chumbani  maana  yake  hata  chumba  chako  ni  CHOO  na  kitakuwa  kinanuka  zaidi  kuliko  choo  cha  kawaida

43.Mimi  nilikuwepo  wakati  sakata  la  Richmond  likijadiliwa.Mimi  nina  ugomvi  wa  muda  mrefu  na  Lowassa.

44.  Mwaka  2010  mimi  nilimtaka  Lowassa  atangaze  Richmond  ni  ya  nani.

45. Leo  tena  namtaka  Lowassa   Lowassa  atoke  hadharani  atangaze  Richmond  ni  ya  nani.  Unaposema  ni  ya  mkubwa, atuambie  mkubwa  gani

46. Ukitaka  kuijua  Richmond  rejea  Ripoti  ya  Mwakyembe. Nampongeza  Mwakyembe  na  Sitta  kujitokeza  hadharan  kuusema  ukweli.

47. Siku  moja  kabla  ya  ripoti  kusomwa, nililetewa  Rushwa  ya  milioni  500  ili  tukaupindishe  ukweli  bungeni  lakini  nilikataa

48. Ripoti  ya  mwakyembe  iliamua   mambo  mawili,  moja; Lowassa  ajipime  au  bunge  lijadili  na  lichukue  hatua.  Lowassa  kuona  hivyo  akaamua  kukimbilia  kujiuzulu  kukwepa  aibu  ya  kung'olewa  na  bunge

49:  Lowassa  haaminiki, ni  muongo  na  hastahili  kuwa  Rais  wa  nchi....

50.  Lowassa  ni  FISADI  na  kama  mimi  ni  muongo  ajitokeze  hadharani  akanushe

51. Anasema  Lowassa  ataleta  maji, mbona  jimbo  lake  la  Monduli  halina  Maji???

52.  Mnasema  Lowassa  kaanzisha  shule  za  kata, iv  mjua  msingi  wa  shule  za  kata?  waandishi  rudini  shule  mkajifunze  upya.

53.Nilifanikiwa  kuijenga  Chadema  na  ikawa  tumaini  jipya  la  watanzania.....Vijana  wangu  wa  Chadema, naomba  niwe  mkweli  propaganda  imekivamia  chama.

54.  Inasikitisha  kuona  CHADEMA  inajazwa kwa mabasi  pale  jangwani .....alafu  mnawadanganya  watu  eti  ni   MAFURIKO

55.  CHADEMA  ya  kipindi  changu  ilikuwa  inakemea  Rushwa. Niambien  leo  chadema  watasema  nini  kwenye  majukwaa?

56. Mnaomtetea  Lowassa  na  nyie  jitokezen  hadharani...mimi  nasema  kwa  sababu  nina  ushahidi  na  sio  lazima  ushahidi  huu  niupeleke  mahakamani.

57. Wenye  uwezo  wa  kumpeleka  Lowassa  Mahakamani  ni  Serikali, na  mwakyembe  alisema  juzi  kuwa  kesi  ya  jinai  haina  kikomo, mtu  anaweza  kushitakiwa  muda  wowote

58. Sitaki  kuingila  swala  la  Babu  Seya, lakini  waliolawitiwa  ni  watoto  waliokuwa  chini  ya  umri. kwa  nini  haki  yao  ipotee?

59.  Rais  hana  mamlaka  ya  kumtoa  Babu  Seya. Lowassa  asiwadanganye.

60.  Kuhusu  swala  la  Masheikh, Sumaye  ndiye  aliyeamuru  mapolisi  wavamie  misikiti  wakiwa  na  mbwa......Watanzania  msikubali  kudanganywa. hizo  ni  propaganda  za  wasaka  urais

61. Masikubali  Rais  Muongo  na  mimi  naapa  ntapiga  kelele  kila  kona  kumpinga  Lowassa.

62.Lowassa  alipokuwa  waziri  mkuu, matatizo  yanayotokea  leo  hayakuwepo?  mapigano  ya  wakulima  na  wafugaji  hayakuwepo?

63.  Lowassa  akiwa  waziri  mkuu  alisababisha  migogoro  mizito  sana  kati  ya  monduli  na  karatu.  Rais  wa  aina  hii  wa  nini?

64.  Naomba  nisiongee  mengi  kwa  sababu  ntakosa  ya  kusema  siku  nyingine.....Nawataka  Lowassa  na  Sumaye  wajitokeze  kunijibu.

65. Siku  nyingine  ntakuja  kuongelea  kuhusu  hisa  za  Lowassa  kwenye  makampuni

66.  Nahitimisha  kwa  kusema  kuwa  Nimestaafu  siasa  na  sina  chama  lakini  nina  nchi, hivyo  ntaendelea  kuwatumikia  watanzania  kwa  jinsi  mungu  alivyonipa  vipawa


67.  Narudia  tena, Sina  chama  na  sitajiunga  na  chama  chochote.

Waandishi  wanauliza  Maswali:
Mwandishi:  Umesema  hujiungi  na  chama  chochote, utawasaidiaje  watanzania?  Rais  gani  unamuunga  mkono?

Mwandishi  Guardian:  Ulisema  Lowassa  atakuwa  assert  kama  atakuja  na  wabunge  na  hao  wenyeviti.  Je  angekuja  kama  assert  ungeyasema  haya  yote?

Mwandishi  binafsi:  Umesema  waliohamia  Chadema  ni  makapi.  Mwaka  1995  Uliihama  CCM,   ukahamia  chadema. Je  na  wewe  ni  KAPI?

Mwandishi-Azam:  Umetangaza  kustaafu  siasa, lakini  bado  unakadi  ya  CCM  na  CHADEMA?  Je  utazirudisha?

Mwandishi  Blog:  Inaonekana  baada  ya  chedema  kukutosa  ndo  maana  unamshambulia  Lowassa, je  ni  kweli?

Majibu:
1. Kadi  ni  mali  zangu  na  siwezi  kuzirudisha. Ya  chadema  nimeilipia  miaka  20,ya  CCM  bado  haijaisha  muda  wake.

2. Kuhusu  urais, mimi  sijagombea  urais  na  sikuchukua  fomu.  sasa  kwa  nini  nikasirike  kisa  wamempa  Lowassa?
Sina  ugomvi  na  Mbowe  na  nakumbuka  alinisaidia  nyumba

3.  Mimi  sio  KAPI....Ili  kuujua  ukweli  unahitaji  kutumia  kigezo. KAPI  ni  yule  aliyekataliwa  na  chama  flani, mimi  sikuwahi  kukataliwa.  Sikuwa  na  uchafu  wowote  wakati  naingia  CCM.

4.  Lowassa  ni  mzigo  tu  hata  kama  angetuletea  hao  watu  wake.....Lowassa  ana  makandokando  mengi. Angetuletea  hao  watu  ndo  tungeamua  tumpokee  au  tusimpokee

5.Mimi  sina  chama  na  sitampigia  kampeni  mtu  yeyote. Mimi  nimefanya  utafiti  kwa Lowassa  pekee, kwamba  taifa  litapata  madhara  gan  Lowassa  akiwa  Rais.....Lowassa  ni  Fisadi.

 -Kazi  yangu  leo  ilikuwa  ni  kuwaambia  watanzania  waachanane  na  ushabiki.Ukihamishia  CHOO  chumbani, manake  harufu  itahamia  huko.
 -Chadema  ya  leo  kwa  sasa  imetekwa  na  Lowassa  na  hawawezi  tena  kuongelea  Ufisadi

                                        Maswali  ya  nyongeza

1.Umesema  waliohamia  chadema  kwa  sasa  ni  sawa  na  mfano  wa  Choo. Je, wewe  ulipohama  hukuwa  choo?  kwa  nini  wewe  uliweza  kukibadili  chama  halafu  akina  Lowassa  washindwe?

Jibu:  Wakati  mimi  nahama  sikuwa  mchafu  kama  hawa  akina  Lowassa  na  Sumaye.