Wagombea urais wa Marekani, Hillary Clinton na Donald Trump
hawakujizuia kutoleana maneno katika hafla ya chakula cha jioni ya kila
mwaka kwa ajili ya kutoa misaada mjini New York, wakati wa kutoa hotuba
zao ambazo ni utamaduni wa kutoa vichekesho kwa kila mmoja anayegombea
urais, nchini Marekani lakini walijikuta wakishambuliana.
Katika mlo huo wa jioni wa kumbu kumbu ya Alfred E.Smith ambao huandaliwa na taasisi ya hisani ya Catholic Charity wagombea hao wawili walikaa meza moja na kutoa maneno ya kuchekesha katika hotuba zao siku moja baada ya mdahalo uliokuwa na ushindani mkali na maneno makali dhidi ya kila mmoja kuwahi kutokea katika historia ya Marekani.
Trump ambaye alianza kuzungumza katika usiku huo alichukua nafasi hiyo kufanya utani juu ya jambo ambalo limezungumzwa sana katika uchaguzi wa mwaka huu kuhusu tabia na mwenendo wake.
Clinton nae kwa upande wake alianza hotuba yake kwa kutoa utani juu ya hali ya afya yake ya hivi karibuni na fedha anazolipwa.
Katika mlo huo wa jioni wa kumbu kumbu ya Alfred E.Smith ambao huandaliwa na taasisi ya hisani ya Catholic Charity wagombea hao wawili walikaa meza moja na kutoa maneno ya kuchekesha katika hotuba zao siku moja baada ya mdahalo uliokuwa na ushindani mkali na maneno makali dhidi ya kila mmoja kuwahi kutokea katika historia ya Marekani.
Trump ambaye alianza kuzungumza katika usiku huo alichukua nafasi hiyo kufanya utani juu ya jambo ambalo limezungumzwa sana katika uchaguzi wa mwaka huu kuhusu tabia na mwenendo wake.
Clinton nae kwa upande wake alianza hotuba yake kwa kutoa utani juu ya hali ya afya yake ya hivi karibuni na fedha anazolipwa.