Tafuta katika Blogu Hii

Ijumaa, 7 Oktoba 2016

Burundi ina mipango ya kujiondoa mahakama ya ICC

Makamu wa Rais wa Burundi Gaston Sindimwo amesema nchi hiyo ina mipango ya kujiondoa kutoka uanachama wa mahakama ya kimataifa ya kushughulikia kesi za uhalifu ya ICC, miezi sita baada ya mwendesha mashitaka mkuu wa ICC Fatou Bensouda kusema watachunguza ghasia zilizuka nchini humo zilizosababisha vifo vya mamia ya watu. Sindimwo amesema wameiandikia mahakama hiyo ya ICC kueleza nia yao ya kujiondoa kutoka mkataba wa Roma kwani wamegundua ni muhimu kujiondoa ICC ili Burundi iwe huru. Nchi hiyo ya Afrika Mashariki ilitumbukia katika mzozo mwaka jana baada ya Rais Pierre Nkurunziza kuamua kugombea muhula wa tatu madarakani kinyume na katiba.

Hakuna maoni: