Tafuta katika Blogu Hii
Ijumaa, 7 Oktoba 2016
Burundi ina mipango ya kujiondoa mahakama ya ICC
Makamu wa Rais wa Burundi Gaston Sindimwo amesema nchi hiyo ina mipango
ya kujiondoa kutoka uanachama wa mahakama ya kimataifa ya kushughulikia
kesi za uhalifu ya ICC, miezi sita baada ya mwendesha mashitaka mkuu wa
ICC Fatou Bensouda kusema watachunguza ghasia zilizuka nchini humo
zilizosababisha vifo vya mamia ya watu. Sindimwo amesema wameiandikia
mahakama hiyo ya ICC kueleza nia yao ya kujiondoa kutoka mkataba wa Roma
kwani wamegundua ni muhimu kujiondoa ICC ili Burundi iwe huru. Nchi
hiyo ya Afrika Mashariki ilitumbukia katika mzozo mwaka jana baada ya
Rais Pierre Nkurunziza kuamua kugombea muhula wa tatu madarakani kinyume
na katiba.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni