Tafuta katika Blogu Hii
Jumatatu, 31 Oktoba 2016
Watoto milioni 300 duniani wanavuta hewa chafu sana
Katika utafiti uliofanywa na Umoja wa Mataifa, karibu watoto milioni 300
wanaishi kwa kuvuta hewa chafu ambayo inaweza kusababisha madhara
makubwa ya kimwili ikiwemo kuharibu ubongo wao. Kulingana na matokeo ya
utafiti wa shirika la kuwahudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF
yaliyotolewa leo Jumatatu, karibu mtoto mmoja kati ya watoto saba
duniani kote anaishi kwa kuvuta hewa ya nje iliyo chafu mara sita zaidi
ya miongozo ya kimataifa, na kusema kwamba uchafuzi wa hewa ni chanzo
kikuu katika vifo vya watoto. UNICEF imechapisha utafiti wake wiki moja
kabla ya kufanyika mazungumzo ya kila mwaka ya Umoja wa Mataifa
yanayohusu mabadiliko ya tabia ya nchi ambayo yatanyika nchini Morocco
katikati ya mwezi Novemba. Kwa mujibu wa UNICEF uchafuzi wa hewa
unasababisha vifo vya watoto laki sita walio chini ya umri wa miaka
mitano kila mwaka na kutishia maisha na mustakabali wa mamilioni ya
watoto, amesema mkurugenzi wa shirika hilo Anthony Lake.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni