Tafuta katika Blogu Hii

Jumamosi, 24 Desemba 2016

Gaddafi: Kumuomboleza Gaddafi

Leo ni miaka mitano tangu kuuawa kwa kiongozi wa muda mrefu wa Libya, Muammar Gaddafi ambaye alituhumiwa na nchi za Magharibi na mashirika ya kutetea haki za kibinadamu kwa ukatili na kukandamiza wapinzani.
Utawala wake uliangushwa kufuatia mashambulio ya ndege za kivita za nchi za Magharibi chini ya mwavuli wa shirika la kujihami la Nato.
Baada ya kuuawa kwake, maelfu ya watu walishangilia kote nchini Libya.
Lakini kadiri miaka ilivyosonga, watu wameanza kumkumbuka na kumuenzi hasa baada ya taifa la Libya kutumbukia katika misukosuko ya kisiasa na vita.
Maelfu ya watu wamekuwa wakitumia taifa hilo kujaribu kufika Ulaya, baadhi wakifariki katika bahari ya Mediterranean. Mataifa ya Ulaya pia yanalalamikia ongezeko la wahamiaji.
Katika nchi za Afrika, wakazi wa nchi ambazo Kanali Gaddafi kwa njia moja au nyingine alichangia kisiasa au kwa miradi ya ujenzi, anakumbukwa.
Mfano nchini Ghan
Karim Mohamed, 46, ambaye ni fundi wa nguo alisema Gaddafi alikuwa kama "masihi wa Afrika".
Alikuwa ameishi Libya wakati wa utawala wa Gaddafi.
"Nchini Libya, kila mtu alikuwa na furaha," anasema.
"Nchini Marekani, kuna watu wanaolala chini ya madaraja. Lakini Libya hilo halikufanyika. Hakukuwa na ubaguzi, hakukuwa na shida, hakuna lililokosekana. Kazi ilikuwa nzuri na kulikuwa na pesa pia. Maisha yangu yako yalivyo sasa kwa sababu ya Gaddafi. Alikuwa masihi wa Afrika."
Jake Wallis Simon alikutana na wanaume wengine wawili ambao pia waliunga mkono Karim.

Ndege iliyotekwa nyara Libya yatua Malta

Ndege moja ya Libya iliyoripotiwa kutekwa nyara ikiwa kwenye safari ya ndani mwa nchi imetua nchini Malta.
Ndege hiyo aina ya Airbus A320 ya shirika la ndege la serikali ya Libya, Afriqiyah, ilikuwa na abiria 118 wakati ilitekwa.
Watekaji nyara wawili waliripotiwa kutishia kuilipua ndege hiyo.
Ndege hiyo ilikuwa safarini kutoka mji wa Sebha kusini magharibi mwa Libya ikielekea mji mkuu Tripoli kabla ya kuelekezwa nchini Malta, kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters.
Karibu watu wote waliokuwa ndani ya ndege wanaripotiwa kuondoka.
Watekaji nyara hao waliondoka ndani ya ndege hiyo na kujisalimisha.
Mmoja wao alikimbia kituo kimoja cha runinga nchini Libya kuwa yeye ni mkuu wa chama chama kinachompendelea kiongozi wa zamani wa Libya Muammar Gaddafi.
Meya wa mji wa Sebha nchini Libya ambapo ndege hiyo ilikuwa ikitokea anasema kuwa watekaji nyara hao wanatafuta hifadhi ya kisiasa.

Jumatatu, 19 Desemba 2016

Rais Rais Magufuli ateua mkuu mpya NIMR

Rais wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amemteua Prof Yunus Mgaya kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) saa chache baada ya kumfuta kazi mkurugenzi wa awali Dkt. Mwele Malecela.
Taarifa kutoka ikulu imesema uteuzi wa Prof Mgaya unaanza mara moja.
Dkt Mwele Malecela, alifutwa kazi siku moja tu baada yake kutangaza kugunduliwa kwa virusi vya Zika nchini Tanzania.
Taarifa ya kufutwa kwake, iliyotolewa na mkurugenzi wa mawasiliano ya ikulu Gerson Msigwa, haikueleza sababu ya kufutwa kazi kwa Dkt Malecela,
Hata hivyo, kulikuwa kumetokea habari za kukinzana kutoka kwake na wizara ya afya kuhusu kuwepo kwa virusi vya Zika nchini Tanzania.
Alitangaza kuwepo kwa virusi hivyo nchini Tanzania siku ya Alhamisi lakini Ijumaa, baada ya habari hizo kuenea kwenye vyombo vya habari, waziri wa afya Ummy Mwalimu akatoa taarifa kukanusha habari hizo.
Dkt Mwele Malecela alikuwa ametangaza kwamba virusi hivyo vimepatikana mkoani Morogoro, Mashariki mwa Tanzania na Mkoani Geita, kaskazini magharibi mwa Tanzania.
Kwa mujibu wake, virusi hivyo viligunduliwa wakati wa utafiti uliofanyika kutokana na uhalisia kuwa kuna mazingira yanayowezesha kuzaliana kwa mbu wanaoeneza virusi hivyo.Kati ya watu 533 waliopimwa wakati wa utafiti huo, asilimia 15.6 waligunduliwa kuwa na virusi vya Zika.
Hata hivyo wizara afya nchini humo, ilitoa taarifa ambapo inakanusha kuwepo kwa virusi hivyo.
"Kama nilivyoeleza mnamo Februari 2016, ugonjwa huu bado haujaingia nchini, na leo pia napenda kuwatoa hofu wananchi kuwa kwa sasa Tanzania haujathibitishwa kuwepo na ugonjwa wa Zika," taarifa ya wizara ya afya imesema.
Wizara hiyo inasema uchunguzi uliofanywa na NIMR ulikuwa wa kuchunguza ubora wa kipimo kipya cha kupima magonjwa ya Zika na Chikungunya.
"Matokeo haya bado yanahitaji kuchunguzwa kwa kina zaidi kupitia vipimo vilivyothibitishwa na Shirika la Afya Duniani," wizara ilisema.

Asili ya Zika

Jina la virusi hivyo linatokana na msitu wa Zika, Uganda ambapo virusi hivyo vilitambuliwa kwa mara ya kwanza 1947.
Wengi wa walioambukizwa aina ya awali ya virusi walikuwa wakipatwa na homa ambayo si kali sana, mwasho na maumivu katika maungio.

Cyril Ramaphosa: Niko tayari kumrithi Jacob Zuma

Makamu wa rais nchini Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ametangaza kwa mara nyingine tena kuwa yuko tayari kumrithi rais Jacob zuma kwenye uongozi wa chama cha ANC. Ndani ya mwaka mmoja, chama cha ANC kitamchagua kiongozi wake, ambaye atakiwakilisha katika uchaguzi wa urais wa mwaka 2019.
"Niko tayari kukitumikia chama cha ANC," alisema Cyril Ramaphosa Jumatano hii Desemba 14 kwenye redio moja nchini Afrika kusini. Hii ni mara ya pili ndani ya muda wa wiki ambapo Makamu wa rais anasema kuwa tayari kuchukua uongozi wa chama cha ANC (African National Congress).
Cyril Ramaphosa alisema kuwa anaendelea kuyasikiliza matawi mbalimbali ya chama cha ANC, akitangaza kwamba atafurahi kama atapata uungwaji mkono.Kwa kawaida Makamu wa rais anatakiwa kumrithi rais wake, lakini Cyril Ramaphosa anakwenda kwa tahadhari. Anajua kwamba kumrithi ni vigumu, kwa sababu chama cha ANC kimegawanyika kati ya wanaomuunga mkono Jacob Zuma na wale wanaompinga.
Ili kuchukua nafasi ya rais anayeshirikiana naye tangu mwaka 2012 kama kiongpzi wa chama cha ANC, Cyril Ramaphosa atapambana na mgombea mwenye ushawishi mkubwa nchini Afrika Kusini, ambaye ni Nkosazana Dlamini-Zuma, Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika na mke wa zamani wa rais Zuma.
Bado hajatangaza rasmi kuwania katika uchaguzi wa urais, lakini tayari anaonekana kufanya hivyo kwa sababu anaungwa mkono na wanaounga mkono Zuma. Nkosazana Dlamini-Zuma pia anawachukulia miongoni mwa washirika wake vijana na Wanawake wa chama cha ANC pamoja na jimbo la KwaZulu-Natal ambapo anazaliwa rais Jacob Zumaya rais. Rais wa Afrika Kusini, mwenyewe anaweza pia kumuunga mkono.

Upinzani wa Gambia wamuonya Yahya Jammeh

Upinzani nchini Gambia wasema Endapo rais anayemaliza muda wake nchini humo Yahya Jammeh atakataa kuondoka Madarakani atachukuliwa kama muasi. Yahya Jammeh alirejelea kauli yake hivi karibuni baada ya kutambua ushindi wa mshindani wake Adama barrow, na kutaka kura zirudi kuhesabiwa upya.
Katikati mwa juma lililopita Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa katika Afrika Magharibi, Mohamed Ibn Chambas, alisema kuwa Rais wa Gambia Yahya Jammeh anapaswa "kuwa tayari kukabidhi madaraka" ifikapo mwezi Januari mwakani.
Bw ibn Chambas alisema Umoja wa Mataifa hautaendelea kufumbia macho viongozi ambao hushindwa na kisha baadaye wanatumia nguvu kwa kuchukua madaraka.
"Upinzani ulishinda uchaguzi, ambao uliku halali" amesema Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa wa Ban Ki-moon katika Afrika ya Magharibi.
Jumanne Desemba 13 Marais wanne kutoka Afrika Magharibi walifanya ziara katika mji mkuu wa Gambia, Banjul na kujaribu kumshawishi Yahya Jammeh kukubali kushindwa katika uchaguzi wa urais na kukabidhi madaraka, bila mafanikio.
Mihula ya miaka mitano ya Bw Jammeh itamalizika Januari 19, Mohamed Ibn Chambas amesema, huku akiongeza kuwa "atakuwa tayari kukabidhi madaraka" tarehe hiyo.
Naye Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, ameendelea kulaani hatua ya jeshi kudhibiti Tume ya Uchaguzi na kuwafukuza wafanyakazi wote ambao kwa sasa hawawezi kwenda kazini.
Awali Ban Ki-moon alimtaka rais Jammeh kuamuru wanajeshi hao kuondoka katika tume hiyo mara moja.
Upinzani nchini Gambia umemuonya Yahya Jammeh ikiwa atakaidi kuachia ngazi, kuwa atachukuliwa kama adui wa nchi hiyo.

Papa Francis atafuta suluhisho kwa mvutano wa kisasa DRC

Papa francis anajaribu kutafuta suluhisho kwa mzozo wa kisiasa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa kuwaita viongozi wa kanisa walokua wanaongoza juhudi za upatanishi kati ya serikali ya Joseph Kabila na upinzani, juu ya hatua za kuchukuliwa baada ya muda wa Kabila wa Jumatatu tarehe 19 unafika.
Mkuu wa Kanisa la Katholiki alichukua hatua hiyo baada ya viongozi wa kidini kukutana na Rais Kabila siku ya Ijuma na kiongozi wa upinzani Étienne Tshisekedi, bila ya kupata ufumbuzi.
Muungano wa upinzani wa "Ressmblemement" unampango wa kuitisha maandamano Jumatatu ambayo Wakongo wengi na Jumia ya kimataifa wanahofu yanaweza kuzusha ghasia nchini humo.
Inaripotiwa kwamba mazungumzo kati ya pande mbili yanatazamiwa kuanza tena siku ya Jumatano.
Kwa upande mwengine afisa wa juu wa Ressemblement anamhimiza Rais Joseph kabila kufikia makubaliano na kundi hilo na kuacha madaraka ili kuruhusu kipindi cha amani cha kukabiliana madaraka.
Muda rasmi wa mhula wa Kabila unamalizika jumatatu tarehe 19.
Freddy Mbuyamu Matungulu kiongozi wa kundi la Nabiso Kongo, "Kongo Yetu", anasema viongozi wa mungano wa Ressemblement wanakutana Kinshasa kuamua utaratibu wa mpito na hali ya baada ya muda wa Kabila kupita.

Wakili wa Jamii Forum anasema mteja wake anakomolewa

Wakili Benedict Ishamakaki anayemwakilisha mahakamani mkurugenzi mtendaji wa Jamii Media ya nchini Tanzania, kampuni inayomiliki mtandao wa Jamii Forum, Maxence Melo alisema mtazamo anaouona katika kesi ya mteja wake ni kama anakomolewa.
Alipozungumza na Sauti ya Amerika-VOA inayotangaza kutoka Washington DC, mwanasheria Ishamakaki alisema ukiangalia chombo kilichomfungulia mashtaka mteja wake, katika barua kutoka kwenye chombo hicho waliandika walikuwa wanasumbuka kumuandikia barua Melo ili kupata taarifa Fulani, kwa maana hiyo kwa maoni yake mwanasheria anaona kama ni “kulipizana kisasi kwamba wewe ulikuwa unatusumbua kupata taarifa ngoja na sisi tukusumbue kupata dhamana”.
Pia aliongeza kuwa mazingira yaliyotengenezwa mahakamani siku ya Ijumaa aliposomewa mashtaka na kupelekea mteja wake kukosa dhamana kwa maoni yake anaona kama “wanachezewa mchezo Fulani”.

DR Congo imo 'hatarini

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo inakabiliwa na hatari kubwa ya kutumbukia kwenye machafuko, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetahadharishwa.
Mjumbe wa UN Maman Sidikou amesema wanajeshi 18,000 wa kulinda amani wa umoja huo ambao wamo nchini humo hawana uwezo wa kukabiliana na ghasia kama hizo iwapo zitazuka.
Maandamano yenye umwagikaji wa damu yamekuwa wakishuhudiwa mara kwa mara kufuatia hatua ya kuahirishwa kwa tarehe ya uchaguzi wa rais.
Upinzani unamtuhumu Rais Joseph Kabila kwa kujaribu kukwamilia mamlaka hata baada ya kumalizika kwa muhula wake Desemba.
Watu kadha walifariki wakati wa maandamano ya kupinga serikali mwezi jana mjini Kinshasa baada ya tume ya uchaguzi kusema haingewezekana uchaguzi ufanyike Novemba.
Makao makuu ya vyama vitatu vya upinzani yalishambuliwa na kuchomwa moto.
"Wadau kutoka pande zote wanaonekana kuwa tayari zaidi na kutumia ghasia kutimiza malengo yao," Bw Sidikou, mkuu wa kikosi cha kulinda amani cha UN kunachojulikana kama Monusco, aliambia baraza la usalama la UN Jumanne.
Ingawa Monusco itafanya kila iwezalo kulinda raia, haina uwezo wa kukabiliana na hatari zote zilizopo."
Aliongeza: "Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeingia kipindi cha hatari kubwa kwa uthabiti wake. Kipindi kijacho kitakuwa kigumu sana, kuna uwezekano wa kufikia pahala ambapo ghasia zitazidi."
DR Congo haijawahi kuwa na rais aliyekabidhi madaraka kwa njia ya amani kwa mrithi wake tangu uhuru miaka 55 iliyopita.
Bw Kabila aliingia madarakani 2001 baada ya kuuawa kwa babake Laurent Kabila.

Maxence Melo apewa dhamana

Mwanzilishi wa Jamii Forums Maxence Melo, ambaye amekuwa akizuiliwa na maafisa wa polisi nchini Tanzania tangu Jumanne wiki iliyopita, amepewa dhamana na mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Masharti ya dhamana ni wadhamini wawili ambao wote walisaini bondi ya shilingi milioni 5 za Tanzania na kwamba Maxenxe hatatoka nje ya Dar es Salaam pasipo kibali cha mahakama.
Bw Melo alishtakiwa kwa makosa matatu Ijumaa.
Makosa hayo ni kuendesha na kumiliki tovuti ambayo haijasajiliwa nchini Tanzania, na kuzuia uchunguzi wa polisi kwa mujibu wa Sheria ya Makosa Kimtandao.
Hakuweza kuwasilisha ombi la kuachiliwa kwa dhamana Ijumaa na alizuiliwa gereza la Keko wikendi.
Kesi itasikilizwa tena tarehe 29 Desemba.

Ijumaa, 16 Desemba 2016

Taarifa za Yahoo zavuja

                                                                    

Kampuni ya mtandaoni ya Yahoo imesema Jumatano kuwa kuvuja kwa taarifa mwezi Agosti 2013 kuliweka taarifa za zaidi ya watumiaji bilioni moja kwenye hatari.
Kampuni ya mtandaoni wa Yahoo imesema Jumatano kuwa kutolewa kwa siri taarifa hapo mwezi Agosti 2013 kuliweka taarifa za zaidi ya watumiaji bilioni moja kwenye hatari. Yahoo imefafanua kuwa wizi huo wa mitandaoni ni tofauti na uliofanyika Septemba wakati kampuni hiyo ilipofichua kuwa taarifa za zaidi ya watumiaji milioni 500 zilivuja 2014.
Yahoo inaamini kuwa mtu asie na idhini Agosti 2013 aliiba taarifa zinazohusina na zaidi ya watumizi bilioni moja wa mtandao huo. Taarifa zilizoibiwa ni pamoja na majina ya watu, akaunti za barua pepe, nabari za simu, siku za kuzaliwa pamoja na mswali ya kiusalama.
Taarifa kuhusu kadi za benki inaaminika kuwa hazikuvuja. Kampuni ya Yahoo yenye makao yake Snnyville California inajiandaa kununuliwa na kampuni ya Verizon kwa dola bilioni 4.8.

Afisa wa chama cha CHADEMA hajulikani aliko

                                                                      
                                                                      Ben Saanane
Sakata la kutoweka kwa afisa wa cheo cha juu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Ben Saanane limechukua sura mpya baada ya chama hicho kutoa tamko rasmi kwamba hawajui alipo msaidizi huyo wa mwenyekiti wa taifa CHADEMA,
Kupitia mwanasheria mkuu wake Tundu Lissu, chama hicho kimeitaka serikali kupitia jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina juu ya mahali alipo Ben Saanane, msaidizi wa mwenyekiti wa taifa upande wa siasa na jamii, anayedaiwa kutoweka tangu Novemba 14 mwaka huu na mara ya mwisho kupata taarifa zake inadaiwa aliwasiliana na mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe.
Tundu Lissu amesema serikali ndio yenye ulinzi na udhibiti mkubwa wa mipaka ya nchi ambapo inao uwezo wa kufahamu kama mtu ametoka nje ya nchi au yupo ndani ya nchi hivyo wanawajibu wa kufanya kila njia ya kumpata Ben Saanane ambaye taarifa za kutoweka kwake kwa mara ya kwanza zilitolewa na ndugu zake wa karibu.
“Wakisema wamemkamata tutawauliza kwa nini wamemkamata na kumshikilia muda wote. Hatumtuhumu mtu yoyote tutauliza masuala ambayo yanahitaji kuulizwa. Huyu Ben Saanane kuna kipindi aliandikiwa barua ya kutishwa,” alisema Lissu.
Katika hatua nyingine CHADEMA pia imetaka uchunguzi wa kutosha juu ya maiti za watu zilizookotwa mto Ruvu ili kujiridhisha aina ya kifo chao licha ya kwamba taarifa za awali zilidai watu hao ni wahamiaji haramu.
Lissu alisema,” Serikali kwa maana ya jeshi la Polisi wanatakiwa kufanya inquest. Inquest ni uchunguzi wa sababu za kifo. Ilikujibu suali hiki kifo kimesababishwa na jinai au ni kifo cha kawaida."
Akanongezea kufafanua kwamba,” wale wataalamu wa uchunguzi (pathologists) lazima wafanye uchunguzi wakitaalamu kutambua huyu mtu amekufa kwa sababu gani.”
Hata hivyo Mwandishi wa VOA Dina Chahali anasema maiti za watu saba wasiojulikana ziliokotwa katika mto Ruvu mkoani pwani Desemba 11 mwaka huu.
Taarifa za awali kutoka polisi zilieleza kwamba miili hiyo inasemekana ni ya wahamiaji haramu, na tayari imezikwa. waziri mkuu Kassim Majali katika maadhimisho ya Maulid hivi karibuni pia aliagiza mamlaka husika kufanya uchunguzi wa vifo hivyo na kutoa taarifa kamili.

Mtandao kubanwa DRC

Kampuni za mitandao katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo zimeamrishwa kufunga mitandao ya kijamii kwanzia Jumapili hii. Hii ni kwa mujibu wa shirika la habari AFP.
Mmoja wa maafisa wa kampuni ya mtandao ameambia AFP kamba wamepokea amri hiyo kutoka kwa serikali kubana mtandao wote. Muhula wa Rais Joseph Kabila chini ya katiba unatarajiwa kumalizika Jumatatu ya wiki ijayo.
Wanaharakati wameanzisha kampeini kwenye Twitter #ByeByeKabila, kama njiya ya kumshinikiza kiongozi huyo kuachia ngazi. Chini ya katiba ya DRC Rais Kabila alistahili kumaliza muhula wake Decemba mwaka huu na kufanyike uchaguzi Mkuu.
Hata hivyo tume ya uchaguzi ilisema haikuwa tayari kuanda uchaguzi. Mazungumzo ya kitaifa ambayo yalisusiwa na vyama vikuu vya upinzani yalipendekeza uchaguzi kuahirishwa hadi mwaka 2018, ambapo Kabila ataongoza kipindi cha mpito.
Licha ya kwamba mahakama ya kuu imeridhia makubaliano hayo, hata hivyo wapinzani wamesema lazima Kabila aondoke madarakani kwanza na kuundwe utawala wa mpito bila yeye kuongoza.
Rais huyo ameahidi kwamba hatagombea mwaka 2018, lakini wapinzani wamepinga hilo. Kumekua na maandamano yaliokumbwa na ghasia na vifo kushinikiza Joseph Kabila kuheshimu katiba ya nchi na kustaafu. Katiba haimkubalii kuwania Urais tena baada ya kumaliza mihula miwili.

Binti wa rais wa zamani wa auawa

                                                                       
        Binti wa Rais wa zamani nchini Msumbiji, Armando Guebuza, Valentina Guebuza ameripotiwa kupigwa risasi na kuuawa katika mji mkuu wa Maputo. Mumewe, Zofino Muiuane amekamatwa na polisi kufuatia tukio hilo lililofanyika Jumatano.
Bi Guebuza alikua na umri wa miaka 36 na imeripotiwa alipigwa risasi mara kadhaa nyumbani kwake na kufariki dunia kutokana na majeraha wakati akipelekwa hospitalini.Mumewe alikamatwa katika moja wapo ya maeneo ya burudani mjini Maputo, kwa mujibu wa gazeti moja.
Valentina Guebuza aliorodheshwa nafasi ya saba miongoni mwa wanawake chipukizi wenye ushawishi Barani Afrika na jarida la Forbes mwaka wa 2013. Alishikilia nafasi ya juu katika kampuni kadhaa za mawasiliano pamoja na biashara zinazomilikiwa na familia.
Mumewe bwana Muiuane ni mfanyibiashara na aliwahi kufanya kazi katika kampuni ya sigara ya 'British American Tobacco'. Wawili hao walifunga ndoa mwaka wa 2014 kwenye sherehe iliyohuhduriwa na wageni 1,700 akiwemo Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma.
Mfalme wa Zwaziland Mswati wa Tatu na binti wa Rais wa Angola Isabel dos Santos. Walijaaliwa na mtoto wa kike mwaka uliopita. Armando Guebuza alistaafu kama Rais mwaka wa 2014 baada ya kuhudumu kwa mihula miwili.

Polisi waendelea kumzuilia mwasisi wa Jamii Forums

                                                                       

aarifa kutoka kwa Jamii Forums inasema Bw Melo alizuiliwa kwa kutotoa taarifa za watumiaji wa mtandao huo.
Alitarajiwa kufikishwa kortini Jumatano lakini hilo halikufanyika.
Badala yake, polisi walifika afisi za Jamii Forums kufanya upekuzi kisha wakawahoji wafanyakazi na kuchukua maelezo ya utendaji kazi wao.
Mashirika ya kutetea haki za kibinadamu yanasema Melo anashikiliwa kinyume cha sheria kwani sheria inataka mtu asishikiliwe na polisi kwa muda unaozidi saa 24 bila kuwasilishwa kortini.
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kilitoa taarifa Jumatano kulaani kuendelea kuwekwa kizuizini kwa Bw Melo.
"Kituo kinalitaka jeshi la polisi kuheshimu katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 ibara ya 1977 inayotoa haki kwa kila mtu kuwa huru na kuishi kama mtu huru," taarifa ya kituo hicho ilisema.
Kupitia taarifa, mratibu wa kitaifa wa shirika la watetezi wa haki za binadamu nchini Tanzania (THRDC) Bw Onesmo Olengurumwa aliwataka maafisa wa polisi kumwachilia huru mara moja Bw Melo kwa sababu "wameshindwa kumfungulia mashtaka kortini katika muda unaotakikana kisheria."
Aliitaka serikali kuhakikisha Sheria ya Makosa ya Kimtandao haitumiwi kukandamiza uhuru wa kujieleza katika mtandao nchini Tanzania.
Wakili wa Melo, Jebra Kambole anasema Ijumaa wana mpango wa kuiandikia Mahakama Kuu ombi la kuiomba iwalazimishe polisi kumpeleka Melo mahakamani hapo afunguliwe mashtaka au aachiliwe

Njia 10 za kujikinga dhidi ya virusi vya Zika

                                                                    

Katika mataifa 20, ambapo virusi hivyo vinaaminika kuchangia kuzaliwa kwa watoto wenye vichwa vidogo, na hasa Brazil, tahadhari imetolewa.
Ni mlipuko wa maradhi ambao unaendelea, na Dkt Anthony Fauci, ambaye ni mtaalamu wa maradhi ya kuambukiza katika Taasisi ya Taifa ya Afya Marekani.
Kuenea huku kwa kasi kwa virusi vya Zika ndiko kwa karibuni zaidi kati ya magonjwa manne ya virusi yanayoenezwa na mbu mataifa ya Magharibi katika kipindi cha miaka 20, anaandika Dkt Fauci kwenye makala katika jarida la kimatibabu lathe New England Journal of Medicine.
Mlipuko huu unafuata mlipuko wa maradhi ya kidingapopo (homa ya dengue), virusi vya Nile Magharibi, na majuzi zaidi, chikungunya. Sawa na maradhi haya, virusi vya Zika pia huenezwa na mbu.
Lakini kinyume na virusi hivyo vingine, hakuna chanjo dhidi ya Zika. Je, ni njia gani iliyopo ya kukabiliana na virusi hivi?

1. Kutumia dawa au mafuta ya kufukuza mbu

Ushauri wa kwanza kabisa ni kuepukana na mbu. Kituo cha Kudhubiti na Kuzuia Maradhi (CDC) nchini Marekani kinapendekeza watu wajipake mafuta yenye kemikali za kufukuza mbu kama vile N, N-diethyl-meta-toluamide (DEET) au picaridin.
Mafuta haya yanafaa kujipakwa mara kwa mara, kwa kufuata maagizo kwenye mikebe, au mtu anapoanza kuumwa na mbu. Mtu anafaa kujipaka baada ya kujipaka mafuta ya kukinga ngozi dhidi ya miali ya jua.
Mafuta mengi ya kufukuza mbu ni salama hata kwa kina mama waja wazito, lakini ni vyema kutafuta ushauri wa daktari kabla ya kuanza kuyatumia.

2. Kuvalia mavazi ya kufunika mwili

Wataalamu pia wanakubaliana kwamba inafaa kuvalia mavazi yanayofunika mwili vyema. Mfano shati au nguo zenye kufunika mikono na pia suruali au long’i ndefu. Mavazi yanafaa kuwa mazito kuzuia mbu kufikia ngozi.
Katika baadhi ya mataifa, mavazi huwekwa dawa maalum aina ya permethrin, ambao hufukuza mbu.
Iwapo utajipaka mafuta ya kufukuza mbu, usijipake na kisha kufunika maeneo uliyojipaka kwa nguo unazovalia.

3. Kuzuia mbu kuingia nyumbani

Ikiwezekana, wataalamu wanawashauri watu walale ndani ya nyumba zilizojengwa vyema na kuwekwa kinga ya kuzuia mbu kuingia.
Usiku, lala chini ya neti zilizotibiwa.
Lakini usitahadhari usiku pekee kwani mbu aina ya Aedes aegypti, wanaoeneza virusi vya Zika, hupenda sana kuuma watu mchana.

4. Chunga mimea inayokua ndani ya nyumba

Ingawa ni muhimu kuzuia mbu kuingia, ni muhimu hata haidi kuzuia mbu kuzaana. Na mbu huhitaji maji.
Watu wanashauriwa kuchunga sana maeneo yenye maji yaliyosimama kwani huko ndiko viluwiluwi wa mbu huwa. Maeneo haya ni pamoja na mikebe, maeneo ya kuwapa mifugo na wanyama wengine lishe, jagi za kuweka maua, vibanda vya kufugia ndege na mimea ya kupandwa ndani ya nyumba.
Ni vyema pia kusafisha mifereji ya maji mara kadha kila wiki, mufunika matangi ya mali na vidimbwi la sivyo kuweka dawa ya krolini (krolini huwafukuza mbu).
Maji ambayo yametulia kwa zaidi ya siku tano yanafaa kutupwa kwa kumwagwa ardhi kavu, kwani viluwiluwi wa mbu watafariki baada ya maji kukauka. Kiasi kidogo tu cha maji kinatosha kwa viluwiluwi hao kukua kwa hivyo, ni vyema kuosha na kukausha vyema maeneo hatari.

5. Kufunika taka

Maeneo ya kutupwa taka mara nyingi huwa na maji na hutumiwa sana na mbu kuzaana.
Ili kuzuia hili, ni vyema kufunika taka, hasa katika mifuko ya plastiki.
Tairi kuukuu na vitu vingine vya ujenzi pia vinafaa kuwekwa vyema, kwani sana huhifadhi maji ambayo yanaweza kutumiwa na viluwiluwi wa mbu.

6. “Kunyunyizia dawa”

Maafisa nchini Brazil, ambako virusi vya Zika vimeenea sana, wanatafakari wazo la kunyunyizia maeneo yaliyoathiriwa na virusi hivyo dawa ya kuua mbu.Hii inachukuliwa kama njia ya dharura kabla ya michezo ya Olimpiki, ambayo itaanza mjini Rio de Janeiro mwezi Agosti.
Hata hivyo, kuna utata kwani njia hii inaweza kuwa na madhara mengine kwenye mazingira na pia kuathiri afya ya wakazi.

7. Kudhibiti mbu

Serikali katika nchi kadha za Amerika Kusini tayari wameanza kampeni ya kuangamiza mbu wanaobeba virusi vya Zika kwa kutumia teknolojia.
Moja ya njia tata zinazopendekezwa ni kueneza mbu waliofanyiwa mabadiliko ya kijeneti ambao hawana uwezo wa kuzaana. Hili litapunguza idadi ya mbu na kuzuia ugonjwa huo kuenea.
Wengine wamejaribu mbinu nyingine, mfano jiji la Itapetim nchini Brazil. Maafisa mjini humo wanatumia samaki kuangamiza mbu huo.
Samaki hao hula mayai ya mbu na hivyo kuzuia kuongezeka kwa idadi ya mbu hao.

8. Vifaa ya kukabili mbu nyumbani

Maafisa wa serikali wanapojaribu kukabiliana na mbu kwa kiwango kikubwa, watu binafsi manyumbani pia wanatumia njia mbalimbali kukabili mbu.
Wanatumia vifaa mbalimbali vya kuwawinga na kuwaua mbu. Mfano ni kutumia kifaa kinachoiga mwili na kutoa hewani ya kaboni dayoksaidi pamoja na joto, ili mbu waingie ndani wakidhani ni binadamu.
Mitambo mingine ya kunyunyiza dawa ya kuua mbu pia inatumiwa, lakini inapingwa na baadhi ya watu kwani inaathiri pia nyuki, vipepeo na wadudu wengine.

9. Kukwepa kusafiri

Wale wanaoishi maeneo ambayo hayajaathirika na virusi hivyo, wanajizuia kusafiri.
CDC imewashauri wanawake waja wazito nchini Marekani kuahirisha ziara zao Amerika Kusini na visiwa vya Caribbean kadiri wawezavyo.
Kituo hicho kimewashauri wanawake wanaopanga kusafiri maeneo hayo kutafuta ushauri wa madaktari kwanza.
Shirika la Afya Duniani (WHO), hata hivyo, halijaunga mkono ushauri huo wa CDC.
“Kwa kutumia ushahidi uliopo, WHO haipendekezi vikwazo vya usafiri au biashara kuhusiana na virusi vya Zika. Lakini kama tahadhari, mataifa mbalimbali yanaweza kutoa mapendekezo mbalimbali ya kiafya na kuhusu usafiri kwa raia wake, kwa kuzingatia utathmini,” WHO imesema.

0. Kuzuia kuenea

Mtu anapoambukizwa, hatua zaidi zinafaa kuchukuliwa kuzuia kuumwa tena na mbu wiki ya kwanza baada ya kuugua, CDC inasema.
Hii ni kwa sababu virusi vya Zika vinaweza kusambazwa kutoka kwa mtu mmoja hadi kwa mtu mwingine kupitia damu baada ya kuumwa na mbu.
Ingawa hatari ya kuenezwa kwa virusi hivi kupitia kujamiiana haijathibitishwa kisayansi, baadhi wanapendekeza watu watumie mipira ya kondomu hadi wiki mbili baada ya kupona.
Aidha, watu wachukue tahadhari kuepusha kuambukizwa virusi hivyo kupitia mate na majimaji ya mwili.

Virusi vya Zika vyagunduliwa nchini Tanzania

                                                                        

Taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu, NIMR imethibitisha kugunduliwa kwa virusi vya Zika nchini Tanzania.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Dkt Mwele Malecela, virusi hivyo vimepatikana mkoani Morogoro, Mashariki mwa Tanzania na Mkoani Geita, kaskazini magharibi mwa Tanzania.
Utafiti huo ulifanyika kutokana na uhalisia kuwa kuna mazingira yanayowezesha kuzaliana kwa mbu wanaoeneza virusi hivyo.
Kati ya watu 533 waliopimwa wakati wa utafiti huo, asilimia 15.6 waligunduliwa kuwa na virusi vya Zika.
Dkt Mwele Malecela ameambia BBC kwamba kwa sasa serikali inaangazia kuzuia wajawazito wasiumwe na mbu ambao wanaaminika kueneza virusi hivyo.
"Bado tunajaribu kuangalia ni aina gani ya virusi vya Zika. Lakini hiyo ni dhahiri, tukizingatia kwamba mbu wanaoambukiza Zika wako nchini kwetu na mazingira yaliyoko nchini kwetu hayatofautiani sana na yale ya Amerika ya Kusini na nchi kama Thailand ambako ugonjwa huo unapatikana," amesema Bi Malecela.
                                                                         

"Ugunduzi huu tumeupata kwa watu na tutaendelea kufanya kazi kuangalia kama tutaupata kwa mbu ambao utatuhakikishia basi kwamba ugonjwa huo ina maana umekuwepo nchini ni vile tu ulikuwa haujaonekana."
"Heri nusu shari kuliko shari kamili, kulielewa jambo na kujua kwamba lipo nchini na kujua kwamba wajawazito wanaweza kuzaa watoto wenye matatizo haya kutatuwezesha kuzuia ugonjwa huyu. Tutahakikisha nguvu zetu za kupambana na mbu wanaoeneza virusi hivi zinaongezeka."
Virusi vya Zika zimekuwa vikisababisha watoto kuzaliwa wakiwa na ubongo uliodumaa na vichwa vidogo katika mataifa ya Amerika Kusini na sana Brazil.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily News la Tanzania, Dkt Malecela, alipokuwa akitangaza matokeo ya utafiti huo mjini Dar es Salaam alisema uchunguzi wao ulionesha kati ya watoto 80 waliozaliwa wakiwa na matatizo ya kimaumbile, asilimia 43.8 walikuwa na virusi vya Zika.
Mapema mwaka huu, serikali ya Tanzania iliwaagiza madaktari wote kuwa macho kuhusu hatari ya virusi hivyo mlipuko ulipotokea nchini Brazil.
Virusi vya Zika huenezwa sana na mbu ingawa kumeripotiwa pia visa vya watu kuambukizwa virusi hivyo kupitia kufanya mapenzi.
Haijabainika iwapo aina ya virusi vya Zika vilivyopatikana Tanzania ni vile ambavyo vimekuwa vikisababisha watoto kuzaliwa na vichwa vidogo Amerika Kusini.
Virusi vya aina hiyo viligunduliwa kwa mara ya kwanza barani Afrika katika visiwa vya Cape Verde mwezi Mei mwaka huu.
Jina la virusi hivyo linatokana na msitu wa Zika, Uganda ambapo virusi hivyo vilitambuliwa kwa mara ya kwanza 1947.
Wengi wa walioambukizwa aina ya awali ya virusi walikuwa wakipatwa na homa ambayo si kali sana, mwasho na maumivu katika maungio.
Lakini kwa aina ya sasa, ambayo mlipuko wake ulianza mwishoni mwa mwaka 2015 nchini Brazil, dalili zake zimekuwa kali na virusi hivyo vinaaminika kusababisha kudumaa kwa ubongo na kasoro nyingine mwilini.
  • 1947: Wanasayansi wanaotafiti kuhusu homa ya manjano msitu wa Zika, Uganda wagundua virusi hivyo kwenye tumbili.
  • 1948: Virusi hivyo vyapatikana kutoka kwenye mbu aina ya Aedes africanus msitu wa Zika
  • 1952: Visa vya kwanza vya binadamu kuambukizwa virusi vya Zika vyaripotiwa Uganda na Tanzania
  • 1960-80: Virusi vya Zika vyapatikana kwenye mbu na tumbili maeneo ya kati Afrika
  • 1960-80: Virusi vya Zika vyapatikana maeneo yenye misitu na mvua nyingi Asia, ikiwemo India, Indonesia, Malaysia na Pakistan
  • 2007: Virusi vya Zika vyaenea nje ya Afrika na Asia, kwanza katika visiwa vya Yap kwenye bahari ya pasifiki
  • 2012: Watafiti wagundua aina mbili tofauti za virusi vya Zika, virusi vyenye asili Afrika na vingine vyenye asili Asia
  • Machi 2, 2015: Brazil yaripoti visa vya watu kuugua kutokana na maambukizi ya virusi vya Zika
  • Julai 17: Brazil yaripoti visa vya watoto kuzaliwa na ubongo uliodumaa na vichwa vidogo
  • Okt. 30: Visa vya watoto kuzaliwa an vichwa vidogo Brazil vyaongezeka
  • Novemba 2015-Januari 2016: Visa vya Zika vyaripotiwa Suriname, Panama, El Salvador,
  • Mexico, Guatemala, Paraguay, Venezuela, French Guiana, Martinique, Puerto Rico,
  • Guyana, Ecuador, Barbados, Bolivia, Jamhuri ya Dominika, Nicaragua, Curacao,
  • Na Jamaica
  • Feb. 2, 2016: Kisa cha kwanza cha Zika kuenezwa Marekani charipotiwa, kikidaiwa kutokana sana na ngono badala ya kuumbwa na mbu.
  • Mei 20: WHO yatangaza kupatikana kwa virusi vya Zika kwa mara ya kwanza Afrika kipindi cha sasa cha mlipuko, katika visiwa vya Cape Verde. Virusi hivyo ni vya aina sawa na virusi vilivyosababisha watoto kuzaliwa na vichwa vidogo Brazil.
  • Agosti 3, 2016: Wataalamu Marekani watangaza kuanza kwa majaribio ya chanjo dhidi ya Zika.

Jumatatu, 12 Desemba 2016

Jammeh akataa kuachia madaraka



Rais Yahya Jammeh aliyeiongoza Gambia kwa kiasi miaka 22  ametangaza ijumaa usiku kwamba hakubaliani tena  na  matokeo yaliyompa ushindi mpinzani wake Adama Barrow na  kutaka uchaguzi mpya ufanyike.Jammeh ametoa onyo kali akiwataka wagambia wabakie majumbani mwao na kutothubutu kuingia mitaani kuandamana.Inaarifiwa wanajeshi walionekana wakiweka vizuizi vya magunia ya mchanga katika maeneo muhimu kote kwenye mji mkuu Banjul hali ambayo inatajwa kusababisha hali ya wasiwasi kote katika taifa hilo la Afrika Magharibi ambalo linaelekea kutumbukia katika mgogoro mpya Wa kisiasa.
Uchunguzi uliofanyika kuhusiana na matokeo ya uchaguzi wa Desemba Mosi yameonesha kutokea kwa dosari zisizokubalika upande wa tume ya uchaguzi alisema Jammeh katika hotuba yake iliyooneshwa kupitia Televisheni ya Taifa na kuonegeza kwamba hatokubali tena kuachia madaraka  kwa mgombea wa upinzani Adama Barrow.Zaidi rais huyo alisema'' kama nilivyokuyakubali matokeo ya uchaguzi kwa nia nzuri naamini kwamba tume huru ya uchaguzi ilikuwa huru na ya kweli na ya kutegemewa,Natangaza kwamba sikubaliani na matokeo kwa hali yoyote.
Jeshi limetawanywa katika mji mkuu  huku Marekani ikilitaka jeshi hilo kuendelea kuheshimu uatawala wa sheria na matokeo ya urais.Tayari upinzani umejibu hatua ya rais Jammeh kwa kumkosoa na kusema kupitia mitandao ya kijamii kwamba anakwenda kinyume na demokrasia lakini pia upinzani umewataka wananchi wagambia wabakie watulivu.Matokea ya hadi sasa yanaonesha Adama Barrow alishinda kwa asilimia 43.29 ya kura wakati Jammeh akipata asilimia 39.64 na idadi jumla ya waliojitokeza kupiga kura ni asilimia.Marekani kupitia balozi wake mjini Banjul imetowa mwito wa Utulivu na kulitaka jeshi liendelee kuheshimu utawala wa kisheria na matokeo ya uchaguzi wa rais.
Desemba 2 rais Jammeh alitoa hotuba iliyovuta hisia kubwa miongoni mwa wananchi wa Gambia baada ya kukubali kushindwa na kuahidi kumpokea madaraka mpinzani wake kwa njia ya amani tangazo ambalo lilizusha vifijo na nderemo katika nchi hiyo.
Lakini sasa Jammeh amegeuza msimamo na kusema kwamba uchaguzi wa Desemba Mosi ulikuwa ndio uchaguzi uliokabiliwa na udanganyifu mkubwa kabisa kuliko chaguzi zote katika historia ya Gambia.Nchi jirani ya Senegal imetoa tamko la kulaani kinachoendelea Gambia huku nchi hiyo ikilitaka baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kukutana kulijadili suala hilo na pia kumtolea mwito Jammeh kuyakubali matokeo na kupisha kipindi cha mpito kwa njia ya amani na kuyakabidhi madaraka.