Tafuta katika Blogu Hii

Jumamosi, 24 Desemba 2016

Gaddafi: Kumuomboleza Gaddafi

Leo ni miaka mitano tangu kuuawa kwa kiongozi wa muda mrefu wa Libya, Muammar Gaddafi ambaye alituhumiwa na nchi za Magharibi na mashirika ya kutetea haki za kibinadamu kwa ukatili na kukandamiza wapinzani.
Utawala wake uliangushwa kufuatia mashambulio ya ndege za kivita za nchi za Magharibi chini ya mwavuli wa shirika la kujihami la Nato.
Baada ya kuuawa kwake, maelfu ya watu walishangilia kote nchini Libya.
Lakini kadiri miaka ilivyosonga, watu wameanza kumkumbuka na kumuenzi hasa baada ya taifa la Libya kutumbukia katika misukosuko ya kisiasa na vita.
Maelfu ya watu wamekuwa wakitumia taifa hilo kujaribu kufika Ulaya, baadhi wakifariki katika bahari ya Mediterranean. Mataifa ya Ulaya pia yanalalamikia ongezeko la wahamiaji.
Katika nchi za Afrika, wakazi wa nchi ambazo Kanali Gaddafi kwa njia moja au nyingine alichangia kisiasa au kwa miradi ya ujenzi, anakumbukwa.
Mfano nchini Ghan
Karim Mohamed, 46, ambaye ni fundi wa nguo alisema Gaddafi alikuwa kama "masihi wa Afrika".
Alikuwa ameishi Libya wakati wa utawala wa Gaddafi.
"Nchini Libya, kila mtu alikuwa na furaha," anasema.
"Nchini Marekani, kuna watu wanaolala chini ya madaraja. Lakini Libya hilo halikufanyika. Hakukuwa na ubaguzi, hakukuwa na shida, hakuna lililokosekana. Kazi ilikuwa nzuri na kulikuwa na pesa pia. Maisha yangu yako yalivyo sasa kwa sababu ya Gaddafi. Alikuwa masihi wa Afrika."
Jake Wallis Simon alikutana na wanaume wengine wawili ambao pia waliunga mkono Karim.

Hakuna maoni: