Wakili Benedict Ishamakaki anayemwakilisha mahakamani mkurugenzi
mtendaji wa Jamii Media ya nchini Tanzania, kampuni inayomiliki mtandao
wa Jamii Forum, Maxence Melo alisema mtazamo anaouona katika kesi ya
mteja wake ni kama anakomolewa.
Alipozungumza na Sauti ya Amerika-VOA
inayotangaza kutoka Washington DC, mwanasheria Ishamakaki alisema
ukiangalia chombo kilichomfungulia mashtaka mteja wake, katika barua
kutoka kwenye chombo hicho waliandika walikuwa wanasumbuka kumuandikia
barua Melo ili kupata taarifa Fulani, kwa maana hiyo kwa maoni yake
mwanasheria anaona kama ni “kulipizana kisasi kwamba wewe ulikuwa
unatusumbua kupata taarifa ngoja na sisi tukusumbue kupata dhamana”.
Pia aliongeza kuwa mazingira yaliyotengenezwa mahakamani siku ya
Ijumaa aliposomewa mashtaka na kupelekea mteja wake kukosa dhamana kwa
maoni yake anaona kama “wanachezewa mchezo Fulani”.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni