Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
inakabiliwa na hatari kubwa ya kutumbukia kwenye machafuko, Baraza la
Usalama la Umoja wa Mataifa limetahadharishwa.
Mjumbe wa UN Maman
Sidikou amesema wanajeshi 18,000 wa kulinda amani wa umoja huo ambao
wamo nchini humo hawana uwezo wa kukabiliana na ghasia kama hizo iwapo
zitazuka.
Maandamano yenye umwagikaji wa damu yamekuwa
wakishuhudiwa mara kwa mara kufuatia hatua ya kuahirishwa kwa tarehe ya
uchaguzi wa rais.
Upinzani unamtuhumu Rais Joseph Kabila kwa kujaribu kukwamilia mamlaka hata baada ya kumalizika kwa muhula wake Desemba.
Watu
kadha walifariki wakati wa maandamano ya kupinga serikali mwezi jana
mjini Kinshasa baada ya tume ya uchaguzi kusema haingewezekana uchaguzi
ufanyike Novemba.
Makao makuu ya vyama vitatu vya upinzani yalishambuliwa na kuchomwa moto.
"Wadau
kutoka pande zote wanaonekana kuwa tayari zaidi na kutumia ghasia
kutimiza malengo yao," Bw Sidikou, mkuu wa kikosi cha kulinda amani cha
UN kunachojulikana kama Monusco, aliambia baraza la usalama la UN
Jumanne.
Ingawa Monusco itafanya kila iwezalo kulinda raia, haina uwezo wa kukabiliana na hatari zote zilizopo."
Aliongeza:
"Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeingia kipindi cha hatari kubwa kwa
uthabiti wake. Kipindi kijacho kitakuwa kigumu sana, kuna uwezekano wa
kufikia pahala ambapo ghasia zitazidi."
DR Congo haijawahi kuwa na rais aliyekabidhi madaraka kwa njia ya amani kwa mrithi wake tangu uhuru miaka 55 iliyopita.
Bw Kabila aliingia madarakani 2001 baada ya kuuawa kwa babake Laurent Kabila.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni