Tafuta katika Blogu Hii

Alhamisi, 19 Januari 2017

Makamu wa rais

                                                                         

Makamu wa rais nchini Gambia Isatou Njie-Saidy amejiuzulu saa chache kabla ya muda wake wa kuongoza kutimia ,AFP imenukuu duru za familia yake.
Waziri wa mazingiura na elimu ya juu pia alijiuzulu,ikiwa ni msururu wa mawazuri kumtoroka bw Jammeh kufuWakati huohuo wakili wa rais Yahya Jammeh ametorokea nchini Senegal baada ya kumuandikia barua rais Jammeh akimtaka kuachilia mamlaka gazeti la Nigeria Primium times limesema.
Edu Gomez alisema kuwa amemfanyia kazi Jammeh chini ya shinikizo chungu nzima .
atia hatua yake ya kukataa kujiuzulu baGazeti hilo pia limenukuu barua hiyo ikisema: Siku ya Jumanne tarehe 17 mwezi Januari 2017, mwanangu na mimi tulifanya uamuzi muhimu kutafuta hifadhi katika taifa jirani la Senegal.Hatua hii tuliona ni muhimu kutokana hofu inayoendelea kutanda na wasiwasi kila wakati.
BBC hatahivyo haijapata uthibitisho huru wa ripoti hiyo.
Bw Gomez alimwakilisha Jammeh katika harakati za kufutilia mbali ushindi wa kiongozi wa upinzani Adama Barrow katika uchaguzi wa tarehe mosi Disemba.
ada ya zaidi ya miongo miwili afisini
                                                                     

Uganda yakanusha tuhuma za Kinshasa kuhusu kundi la M23

Serikali ya Kampala yakanusha tuhuma kuhusu kundi la waasi wa zamani wa M23 Mashariki mwa DR Congo
Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo alifahamisha kutiwa wasiwasi na uwepo wa waasi wa zamani wa kundi la M23 Mashariki mwa nchini.
Kwa upande wake serikali ya Kampala immekanusha uwepo wa waasi hao katika ardhi ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Serikali ya Kinshasa ilifahamisha wanamgambo wapatao 150 wa kundi la M23 walingia mashariki mwa Jamhuri ya kşdemokrasia ya Congo.

Putin,Merkel na Hollande,Wafanya mazungumzo

Rais wa Urusi Vladimir Putin,Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na rais wa Ufaransa Francois Hollande wamefanya mazungumzo ya simu

Rais wa Urusi Vladimir Putin,Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na rais wa Ufaransa Francois Hollande wamefanya mazungumzo ya simu kuhusu utatuzi wa masuala ya Ukraine.
Viongozi hawa watatu wamejadili jinsi ya kuisaidia nchi ya Ukraine kutatua matatizo yake.
Mkutano pia uligusia kuendeleza kwa makubaliano waliofanya na nchi hiyo mnamo Oktoba mwaka jana mjini Berlin.
 Kwa mujibu wa habari Mgogoro kati ya serikali ya Ukraine na kundi la Pro Russian Separatist lazima utatuliwe kwani unazidi kusababisha maafa.
Mpaka sasa watu takriban 9750 wamepoteza maisha kutokana na mgogoro huu.

Joto laongezeka zaidi duniani

Kwa kipindi cha miezi kumi na mbili,Hali ya joto duniani imefikia kiwango cha juu zaidi kilichowahi kutokea kwa miaka mitatu mfululizo.
Utafiti uliofanywa na Umoja wa Mataifa na kusaidiwa na shirika la uchunguzi wa masuala ya anga ( NASA), umebaini kuwa wastani wa joto kabla ya mapinduzi ya viwanda ilikuwa ni kipimo cha celsius 1.1.
Madhara yanayotokana na hali hii ni pamoja na ukame huko nchini India, na kuyeyuka kwa kiwango kikubwa cha barafu katika ukanda wa Arctic.
Wataalamu wametaja sababu za kuongezeka kwa joto duniani kuwa ni pamoja na kuongezeka kwa shughuli za kibinadamu kama vile shughuli za viwanda zinazochangia kiasi kikubwa cha gesi chafu na hali ya matukio ya asili maarufu kama El Nino yanayosafirisha joto kutoka katika bahari ya pasifiki.
Huu ni mmoja kati ya miaka 16 ya joto zaidi kuwahi kutokea, hali hii imetokea tena karne hii.

Mtu wa mwisha o kutembea kwenye Mwezi, afariki dunia

                                                                   

Mwana anga wa Marekani Gene Cernan, aliyekuwa binadamu wa mwisho kutembea kwenye Mwezi, amefariki dunia akiwa na miaka 82.
Shirika la anga za juu la Marekani Nasa limesema limehuzunishwa sana kumpoteza mwana anga huyo mstaafu.
Cernan alikuwa mmoja wa watu watatu pekee waliowahi kwenda Mwezini mara tatu na ndiye binadamu aliyeukanyaga Mwezi mara ya mwisho kabisa, mwaka 1972.
Maneno yake ya mwisho aliyoyasema kabla ya kuondoka kwenye Mwezi yalikuwa: "Tunaondoka jinsi tulivyokuja na, Mungu akitujalia, tutarejea na amani na matumaini kwa binadamu wote."
Alikuwa kamanda wa chombo cha anga za juu cha Apollo 17 wakati huo.
Ni watu 12 pekee waliowahi kutembea kwenye Mwezi, na kati yao ni sita pekee ambao bado wako hai.
Kupitia taarifa, familia ya Cernan imesema alifariki dunia Jumatatu baada ya kupata matatizo ya kiafya.

Majeshi ya Afrika tayari kuingia Gambia

                                                                              
                                                            Mkuu wa majeshi Ousman Badjie
Majeshi Senegal yakiungwa mkono na mengine ya Afrika yameweka kambi katika  mpaka  na  Gambia baada ya rais Yahya Jammeh kukataa  kuachia  madaraka wakati huu ambapo akiendelea kutengwa na maafisa wa serikali yake
Mkuu wa majeshi wa rais  Jammeh amesema jeshi lake halitoingia katika mapambano wakati majeshi hayo ya kigeni yatakapoingia katika ardhi ya taifa hilo wakati huu ambapo pia rais wa Mauritania ameondoka mjini Gambia baada ya kushindwa jitihada za mwisho kuachia madaraka kwa hiari. Mkuu wa majeshi Ousman Badjie amenukuliwa na vyombo vya habari akiosema "Hatuwezi kujihusisha kijeshi". Akiuita kuwa ni mgogoro wa kisiasa.
Afisa huyo wa ngazi ya juu kabisa katika jeshi la Gambia aliongeza kusema hawawezi kuwaingiza wanajeshi wao katika mapigano yakupuuzi. Anawapenda watu wake, na kama wanajeshi wa Senegal wakiingia "tutasalia kama hivi", akionesha mikono juu kama ishara ya kusalimu amri.
Muda ya Jammeh madarakani umemalizika
Muda wa Jammeh umefikia kikomo usiku wa manane lakini bado amekaidi kuachia ofisi baada ya kushindwa na mpinzani wake Adama Barrow katika uchaguzi wa mwezi uliopita, na kuzusha mashinikizo ya kumataka aachie ngazi kutoka kwa mataifa ya Afrika Magharibi, baada ya wiki kadhaa za kushindwa kwa mazungumzo ya kidiplomasia.
Nigeria imepeleka majeshi na ndege za kivita Senegal, taifa ambalo jeshi lake kwa wakati huu limekusanyika katika mpaka wa Gambia. Mashuhuda wanasema hali ya utulivu imetawala usiku wa kuamkia leo katika mji mkuu wa Bajul, ingawa majeshi yametawanywa pia katika mitaa ya mji huo.
Baraza la usalama kujadili Gambia
Chanzo kimoja cha kidiplomasia kimesema baraza la usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kukutana leo kuridhia takwa la Afrika Magharibi lenye kumtaka Jammeh kukabidhi madaraka. Lakini msemaji wa Jeshi la Senegal, Kanali Abdou Ndiaye aliliambia shirika la habari la Ufaransa AFP kwamba kama suluhu za kisiasa zikishindwa tutafanya operesheni za kijeshi nchini Gambia.
Baada ya mazungumzi yake na Rais Jammeh, mjini Banjul, ambayo amesema yanamatumaini ya kufikia suluhisho la amani la kisiasa mpatanishi Rais wa Mauritania Mohamed Ould Abdel Aziz amewasili mjini Dakar, ambako amekutana na Barrow, akiwa amepatiwa hifadhi, na vilevile rais wa Senegal Mack Sally. Hayo ni kwa mujibu wa radio moja binafsi nchini humo.
Naye mkuu wa kamati ya maandalizi ya kuapishwa kwa rais mteule Adama Barrow, James Gomez, hafla ambayo ilipaswa kufanyika katika uwanja mkuu mjini Banjul amesema  kwa hivi sasa hafla hiyo imeahirishwa. Rais wa Gambia mwenye umri wa miaka 51 alitangaza hali ya hatari hapo Jumanne, iliofuatiwa na taarifa kuwa bunge limemruhusu kubakia madarakani kwa miezi mitatu .
Makamu wake wa rais Isatou Njie-Saidy amejiuzulu, sambamba na mawaziri  kadhaa  na mkuu wa jeshi la polisi kuacha utiifu, ikiwa ni katika tukio la karibuni la kujitenga na Rais Jammeh.

M23 warejea Congo

                                                                                

Waasi wenye silaha nchini Congo wameingia tena nchini humo kutoka katika nchi jirani ya Uganda, na kuzusha hofu kwamba mapigano ya chini kwa chini ambayo yalifikishwa mwisho mwaka 2013 yanaweza kuanza tena.
Karibu  wapiganaji  200  wa  kundi  la  M23 , kundi  la  Watutsi  walio jamii  ya  wachache  lililoshindwa  na  jeshi  la  Jamhuri  ya kidemokrasi  ya  Congo  miaka  mitatu  iliyopita , wamewasili  kutoka Uganda  na  kukamata  kijiji  kimoja  kaskazini  mwa   jimbo  la  Kivu ya  kaskazini, msemaji  wa  serikali  ya  Congo Lambert Mende ameliambia  shirika  la  habari  la  Ufaransa  afp.
Mende  amesema  jeshi  la  Congo  linapambana  na  vikosi  viwili vilivyopelekwa  katika  kijiji  cha  Ishasha ambavyo  vilitarajiwa  kuwa nchini  Uganda  chini  ya  uangalizi  wa  maafisa  wa  nchi  hiyo.
"Ni  vipi  majirani  zetu  wa  Uganda , ambao  tuna  mipaka  nao wakiwajibika  kabisa, wameweza  kuruhusu   watu  ambao  walikuwa wanaishi  katika  makambi  ya  wakimbizi  kuvuka  mpaka  na  silaha , hadi  katika  ardhi  yetu?"  ameongeza.
Serikali  ya  Congo  imesema  jenerali  wa  zamani  wa  jeshi, Sultani Makenga , anaongoza  moja  kati  ya  batalioni.  Hakuna  msemaji wa  jeshi  alipatikana   kuthibitisha  mapigano  hayo  na  kundi  la M23. Omar Kavota, mkurugenzi wa  kituo  cha  kuhimiza  amani , demokrasia  na  haki  za  binadamu  amesema  Jumapili  kwamba vyanzo  katika  kijiji  cha  Ishasha  vimethibitisha  kuwapo  kwa wapiganaji  wa  kundi  la  M23  lakini  amesema "hakukuwa  na mapigano  ama  mapambano  bado".
                                                                                         

Hatari ya  mapigano
Majimbo  yenye  utajiri  mkubwa  wa  madini  nchini  Congo yameathirika  na  miaka  kadhaa  ya  mzozo  mbaya  kabisa, wakati mataifa  jirani  yakiunga  mkono  makundi  ya  waasi  katika  vita  vya wenyewe  kwa  wenyewe   dhidi  ya  mamlaka  ya  mjini  Kinshasa, na  sasa  wanamgambo  wanaotembea  hovyo  katika  eneo  hilo wanazusha  mapigano  makubwa  na  kuwatisha  raia.
Baada  ya  kushindwa  katika  mapigano  ya  mwaka  2013  na   jeshi la  Congo  na  majeshi  ya  Umoja  wa  mataifa , kundi  la  M23 lilikubali mpango  wa  kuweka  silaha  chini  na  kunyang'anywa silaha,  kuvunja  vikosi  vyao  na  kujumuishwa  katika   jamii  ya watu  wa  Congo.
Lakini  kurejea  kwa  waasi  hao  wa  zamani  kulikwama  , ambapo chini  ya  wapiganaji  200  kati  ya  wapiganaji karibu  1,900 waliokuwa  wakihifadhiwa  nchini  Uganda  na  13  kati  ya  mamia waliondoka  nchini  Rwanda  na  kurejea  Congo.
Wakati  wa  vita  vya  wenyewe  kwa  wenyewe  nchini  Congo maafisa  waliishutumu  Rwanda  na  Uganda  kwa  kuruhusu  waasi kutumia  ardhi  zao  kama  sehemu  ya  kuanzisha  mashambulizi yao. Hivi  karibuni  kabisa, wameyalaumu  mataifa  hayo  kwa  kuwa na  nia  mbaya  ya  kuwaruhusu wahalifu  kutembea  huru  kabisa , badala  ya  kuwarejesha  ili  kufikishwa  mahakamani  nchini  Congo.
Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Uganda Henry Okello Oryem , akizungumza  na  shirika  la  habari  la  afp  mjini  Kampala , alikana vikali  kuwaunga  mkono  waasi  wa  M23  ambao  wamevuka mpaka.

Jumanne, 3 Januari 2017

Netanyahu ahojiwa kwa tuhuma za rushwa

                                                                          


Polisi nchini Israel wamemhoji Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, kuhusu madai ya kupokea zawadi kutoka kwa wafuasi na wafanyabiashara mbalimbali kinyume na sheria.
Netanyahu alihojiwa kwa muda wa saa tatu katika makazi yake mjini Jerusalembaada ya kutuhumiwa kupokea "zawadi haramu," alisema msemaji wa polisi katika taarifa yake.
"Hakuna maelezo zaidi yanayoweza kutolewa kwa wakati huu," ilisema taarifa hiyo.
Wizara ya Sheria pia imethibitisha katika taarifa yake kuwa Netanyahu alihojiwa na kitengo cha polisi ya kupambana dhidi ya rushwa cha "Lahav 443".
Lengo la mahojiano haya ni kubaini ikiwa Netanyahu, alipokea zawadi hizo kinyume na sheria kutoka kwa matajiri wanaomuunga mkono.
Uchunguzi huu pia unalenga kubaini ikiwa Netanyahu alipokea Maelfu ya fedha kutoka kwa wafanyibiashara kutoka nje ya nchi lakini, pia Waisraeli wanaomuunga mkono.
Benjamin Netanyahu alihojiwa kwa amri ya mwanasheria mkuu wa Israel.
Hata hivyo Benjamin Netanyahu alikana kuhusika katika jambo hilo, huku akisema malalamiko yanayotolewa dhidi yake kuwa alikua akipokea zawadi kutoka kwa wafanyabiashara mbalimbali ni uzushi mtupu na kusema kuwa maadui wake wa kisiasa wanatumia mbinu hiyo kuiangusha serikali yake.
Licha ya tuhuma hizi, Netanyahu amekiri kuwa mwaka 2001, alipokea Dola za Marekani 40,000 kutoka kwa tajiri kutoka Ufaransa Arnaud Mimran, wakati hakuwa Ofisini, fedha alizotumia kuinua sifa ya Israel nje ya nchi.
Netanyahu na mke wake Sara wamehusishwa katika kashfa mbalimbali kipindi cha nyuma, ikiwemo tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za serikali.

Mashekhe 18 washikiliwa na polisi-Uganda

                                                                    

Idadi ya mashekhe waliouawa inasadikiwa imefikia 17, na kati yao wanne ni mashekhe maarufu nchini Uganda.
Mashekhe 18 wamekamatwa wiki iliyopita na polisi nchini Uganda kufuatia wimbi la mauaji ya kushangaza ya mashekhe nchini humo.
Kwa mujibu wa duru za habari jijini Kampala kuna makundi mawili yanayo gongana katika misikiti miwili mikubwa, mmoja uko eneo la Nakasero na mwingine mjini Kampala.
Akiongea na VOA, Sheikh mmoja kwa sharti kutotajwa jina amesema kwamba Baraza Kuu la Umoja wa Waislamu Uganda limegawanyika katika makundi matatu. Lakini makundi mawili ambayo yaliamua kujitoa katika baraza hilo hayatambuliwi na serikali.
“Kundi ambalo linatambuliwa na serikali ni lile ambalo ofisi zake ziko Old Kampala, mengine ambayo yako Kibuli na Nakasero hayatambuliwi,” alifafanua.
Pande hizo zimehasimiana na zimeendelea kushutumiana na inasemekana zimeshindwa kufikiasuluhu. Mpaka sasa jumla ya mashekhe waliotiwa kizuizini ni 45.
Lakini wachambuzi wa mambo ya dini wanasema tatizo lililopo linafungamana na ushindani wa makundi haya mawili ambayo sasa imechukua sura mpya baada ya baadhi ya viongozi wa dini kuuwawa.
“Kinachotokea hivi sasa kila wakati sheikh anapouliwa kutoka upande mmoja, pande nyingine zinanyoosha vidole kulaumu kundi jingine na hivyo polisi huenda na kuwakamata watu hao,” alielezea kwa undani.
Mtu mmoja ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema hadi hivi sasa idadi ya masheikh waliouwawa imefikia 17, na kati yao wanne ni masheikh maarufu nchini Uganda.
Lakini habari tulizopokea kutoka katika duru za kiislamu nchini Uganda zinasema imekuwa vigumu kwa Baraza Kuu la Umoja wa Waislam Uganda kusuluhisha mgogoro huu kutokana na kugawanyika kwa chombo hicho katika makundi matatu.
“Baraza limegawanyika na kumekuwa na pande ambazo zinavutana,” alisema mtoaji habari kwa sharti jina lake lisitajwe.
Lakini katika juhudi za kutafuta suluhu kati ya makundi haya bunge la Uganda lilijaribu kuingilia kati suala hili mara tu pale mauaji yalipoanza na kuiomba polisi kuchukua hatua mara moja.
Moja ya kero za wabunge waliokuwa wanajadili mada hii bungeni ilikuwa kitendo cha polisi kuvamia misikiti na kuifunga mashariki mwa Uganda, kitu ambacho kilikuwa kinaingilia uhuru wa kuabudu, alisema mmoja wa wabunge hao.
Lakini kuna pia taarifa kwamba kukamatwa kwa mashekhe kunatokana na kifo cha meja Sulaiman Kigundu aliyeuwawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana. Dereva wake pia aliuwawa katika tukio hilo.
Chanzo cha habari hii kinaeleza kuwa mashekhe hawa wanashukiwa kuwa wamehusika na kifo hicho.
“Tunaelezwa na jeshi la polisi kwamba wameshikiliwa ili kusaidia katika upelelezi wa vifo hivyo,” alisema moja wa waumini mjini Kampala.
Kigundu alikuwa mmoja wa wapiganaji wa chama cha Allied Demokratic Forces ambaye serikali ya Uganda ilimpa msamaha ili ajisalimishe.
ADF ni kundi la waasi kinachoipinga serikali ya Uganda na kinatambulika kama kundi la kigaidi.

Askofu aliyewapatia silaha Wapalestina afariki

                                                                                 

Aliyekuwa askofu mkuu wa kanisa katoliki mjini Jerusalem ambaye alipatikana na hatia ya kuwapelekea silaha wapiganaji wa Palestina amefariki akiwa na umri wa miaka 94.
Hilarion Capucci alihudumia kifungo cha miaka 12 jela nchini Israel kabla ya Vatican kuingilia kati na kusaidia kumwachilia huru.
Alikuwa na historia ya uanaharakati unaohusishwa na mgogoro unaondelea mashariki ya kati.
Rais wa Palestina Mahmoud Abbas alituma risala za rambi rambi akimtaja kuwa alikuwa mpiganiaji wa uhuru.
Vatican ilithibitisha kifo chake siku ya Jumatatu ,lakini haikusema kiini cha kifo hicho ama hata kutoa maelezo.
Capucci alizaliwa katika mji wa pili kwa ukubwa nchini Syria Allepo mwaka 1922.
Alitawazwa kuwa kasisi wa kanisa la Allepo mwaka 1947 kabla ya kuteuliwa kuwa Askofu mkuu wa Jerusalem.
Mwaka 1974, alikuwa akisafiri kutoka Beirut kuelekea Jerusalem ndani ya gari lililokuwa na nambari za mwanadiplomasia wakati liliposimamishwa na vikosi vya usalama vya Israel.
Ndani yake kulikuwa na bunduki nne aina ya Kalashnikov, bunduki nyengine mbili aina ya pistol , silaha na maguruneti yalionuia kupewa wanachama wa PLO.
Capucci alisisitiza kuwa ailazimishwa kusafirisha silaha hizo ,lakini mahakama ya Israel ilimpata na hatia ya kusafirisha silaha na kumuhukumu miaka 12 jela.
Aliachiliwa huru mwaka 1977 baada ya ombi la papa John Paul wa sita.
Capucci alisalia katika vyombo vya habari baada ya kuachiliwa kwake , akijaribu kuwa mpatanishi wa raia wa Marekani waliotekwa nchini Iran .
Ijapokuwa aliwakera baadhi ya mateka wa Marekani na matamshi yake wakati alipowatembelea ili kuangalia hali yao 1980, alihusika pakubwa katika usafirishaji wa miili minane ya wanahewa wa Marekani waliofariki katika jaribio la kuwaokoa wenzao.
Mwaka 1990, alisafiri hadi nchini Iraq chini ya uongozi wa Saddam Hussein ili kusaidia kuachiliwa huru kwa raia 68 wa Itali waliozuiliwa kuondoka nchini humo kufuatia uvamizi wa Kuwait.
Miaka 10 baadaye Capucci aliongoza ujumbe wa viongozi wa dini na wataalam nchini Iraq kwa umoja dhidi ya vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
Mwaka 2010, alikuwa ndani ya meli ya Mavi Marmara wakati meli hiyo ya Uturuki ilioposimamishwa na makamanda wa Israel, iliposhiriki katika usafirishaji wa misaada ili kujaribu kukiuka kizuizi cha Ukanda wa Gaza.
Wanaharakati 10 wa Uturuki , mmoja wao akiwa raia wa Marekani mwenye uraia wa mataifa mawili ,waliuawa na makumi kujeruhiwa wakati ghasia zilipozuka baada ya makamanda hao kuingia katika meli hiyo,wakishuka kutoka kamba za helikopta.
Capucchi anasema kuwa uvamizi huo haukukubalika.

Jumatatu, 2 Januari 2017

Mwaka mpya na uongozi mpya Umoja wa Mataifa

                                                                          

Guterres ameahidi kufanya kazi na uongozi wa Trump ingawaje kumekuwepo na msuguano na atajaribu kushirikiana katika kuondoa "changamoto mbali mbali" ambazo Marekani na Umoja wa Mataifa zitakabiliana nazo siku za usoni.
Katibu Mkuu mpya wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres tayari ameshachukua madaraka ya juu katika taasisi ya dunia Jumapili, baada ya Ban Ki Moon kumaliza muda wake Desemba 31 saa sita usiku.
Guterres, ambaye ni waziri mkuu wa zamani wa Ureno na aliyekuwa kamishna wa idara ya Umoja wa Mataifa ya kuhudumia wakimbizi, ameiambia taasisi hiyo ya dunia katika hotuba yake kuwa suala la namna ya kuwasaidia watu waliokumbwa na migogoro na vita lina uzito mkubwa moyoni mwake.
Aliongeza kuwa wananchi wasio na hatia wanaendelea kukabiliwa na nguvu za kikatili, wanauawa na kujeruhiwa, wanatobanduliwa katika makazi yao na kutumbukizwa katika ufukara. Alilalamika kuwa hata mahospitali na misafara ya misaada haiko salama tena kutokana na vita.
Guterres amewataka wafanyakazi wenzake Umoja wa Mataifa "kukubaliana katika azimio moja la pamoja la mwaka mpya: Hebu basi tukubaliane kwamba amani ndiyo kitu cha kwanza."
"Hili lionekane kutoka kwenye mshikamano wetu na upendo wetu katika maisha yetu ya kila siku na mazungumzo na kuheshimiana katika migawanyiko yetu ya kisiasa," alisema.
Guterres ameahidi kuwa ni mwenye kuiunganisha dunia wakati rais mteuli wa Marekani, Donald Trump ameeleza wasi wasi wake kuwa Umoja wa Mataifa haina mashiko.
Hata hivyo Guterres ameahidi kufanya kazi na uongozi wa Trump ingawaje kumekuwa na msuguano na atajaribu kushirikiana katika kuondoa "changamoto mbali mbali" ambazo Marekani na Umoja wa Mataifa watakabiliana nazo siku za usoni.
Ban, ambaye amemaliza muda wake amewaambia wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa katika hotuba yake ya mwisho aliyoitoa Ijumaa "anajivuna sana" kufanya kazi nao kwa miaka kumi iliyopita.
Amewasihi waweke vipaumbele vyao na kuendelea kufuata malengo yao ya juu ya mambo ya maendeleo endelevu, kama vile mabadiliko ya tabia nchi, kuwawezesha wanawake, kuwawezesha vijana na mambo mengi mengineyo.

China kupiga marufuku biashra ya pembe za ndovu

Serikali ya China imetangaza kwamba itapiga marufuku biashara ya pembe za ndovu na viwanda vya kuchonga pembe hizo ifikapo mwisho wa mwaka 2017.
Baraza la mawaziri la China katika taarifa yake hapo Ijuma, limeeleza kwamba “ili kulinda vyema ndovu na njia bora ya kupambana na biashara haramu China itasitisha hatua baada ya hatua viwanda na uuzaji wa pembe kwa ajili ya biashara, ifikapo mwisho wa 2017.”
China imekua ikikabiliwa na shinikizo kutoka Jumuia ya Kiamtaifa kukomesha utumiaji wa bidhaa za pembe. Na mwezi Machi baada ya mkutano kati ya marais Barack Obama na Xi Jinping, serikali ya Bejing ilieleza kwamba itapanua marufuku ya pembe na bidhaa za pembe zlizoagiziwa kutoka nje kabla ya 1975.
"Haya ni mabadiliko makubwa kwa ndovu wa afrika", alisema Aili Kang, mkurugenzi wa kitengo cha Asia cha Tasisi ya kulinda Wanyamapori iliyoko New York. “Nina fahari kubwa kwa nchi yangu kuonesha uwongozi ambao utasaidia kuhakikisha kwamba ndovu wana uwezo hivi sasa ya kunusurika na kutotoweka duniani.”
Shirika la habari la China Xinhua linaeleza kwamba marufuku hiyo itasababisha kufungwa kwa viwanda 34 na vituo 143 vya bishara vilivyoidhinishwa.
Biahsra ya peme ilipigwa marufuku 1989 na mkataba wa kimataifa chiniya shirika la CITES. China ndio soko kuu la duniani la biashara ya pembe za ndovu.

Korea Kaskazini kutengeza kombora la masafa marefu

Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amesema kuwa taifa lake linakaribia awamu ya kutengeza kombora la masafara marefu ambalo lina uwezo wa kubeba bomu la nuklia.
Katika hotuba ya kuukaribisha mwaka mpya iliopeperushwa hewani katika runinga ya taifa Bw Kim amesema kuwa Korea Kaskazini imeimarika kama taifa lenye uwezo wa kinyuklia mwaka 2016.
Pyongyang imefanya majaribio mawili ya kombora la kinyuklia katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita ikiwa ni mojawapo ya majaribio yake makubwa kufikia sasa.
Hatua hiyo ilizua shutuma mbalimbali na kuvutia vikwazo vya kimataifa .
Haijulikani taifa hilo imekaribia kivipi kutengeza kombora la Kinyuklia ambalo linaweza kurushwa na kufika Marekani.

Yahya Jammeh afungia kituo kinachomkosoa

Mamlaka nchini Gambia imekifunga kituo kimoja cha habari ambacho kimekuwa kikimkosoa rais wa taifa hilo Yahya Jammeh.
Maafisa wa Ujasusi waliagiza kituo cha habari cha Teranga FM kufungwa bila ya kutoa sababu ,alisema Emil Touray mkuu wa vyombo vya habari nchini humo.
Hii ni ishara ya kwanza ya vita dhidi ya vyombo vya habari tangu bwana Jammeh kukataa kushindwa katika uchaguzi wa Disemba mosi.
Bwana Jammeh alichukua mamlaka katika mapinduzi ya serikali mwaka 19194.
Awali alikuwa amekubali kushindwa na mfanyibiashara Adama Barrow, lakini akaenda mahakamani ili kupinga matokeo hayo,akisema uchaguzi hu ulikumbwa na udanganyifu.
Tume ya uchaguzi nchini humo imesema kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru.

Trump na Ngueso kuijadili Libya

Rais Denis Sassou Ngueso wa Jamhuri ya Kongo atakutana na rais mteule wa Marekani, Donald Trump, kuujadili mgogoro wa kisiasa unaoendelea nchini Libya, pamoja na masuala mengine yanayolihusu bara la Afrika. Msemaji wa Nguesso, Thierry Moungalla, amethibitisha  taarifa hiyo kupitia mtandao wa Twitter. Wawakilishi wa Trump, anayetarajiwa kuanza rasmi majukumu yake Januari 20, hawakuwa tayari kuthibitisha mara moja juu ya kuwepo kwa mkutano huo. Libya imekuwa ikikabiliwa na mgogoro wa kisiasa kufuatia pande mbili za kiserikali nchini humo kuhasimiana huku makundi mengine yaliyo na silaha nayo pia yakipambana kuwania madaraka. Mapema mwezi huu, Umoja wa Mataifa ulielezea juu ya mgogoro wa kibinadamu nchini Libya, ambao unazidi kuyafanya mapambano dhidi ya wahamiaji haramu kuwa magumu.