Tafuta katika Blogu Hii

Jumamosi, 26 Novemba 2016

,Fidel Castro amefariki dunia

                                                                     

Kiongozi mashuhuri ,mwanamapinduzi , aliekuwa  Rais  wa  Cuba,Fidel  Castro  amefariki  dunia  akiwa  na  umri  wa miaka 90.Taarifa juu ya kifo cha mwanamapinduzi  huyo ilitolewa, na ndugu  yake,  Rais Raul  Castro kwenye  televisheni  ya  serikali alisema: " Wapendwa  watu wa Cuba,  marafiki wa Amerika yetu na  dunia  nzima, nikiwa  na majonzi mazito,  nawapa  taarifa ,kwamba  kamanda  mkuu wa mapinduzi  ya Cuba,Fidel Castro Ruz  amefariki  dunia."
Fidel  Castro  aliiongoza  Cuba, baada  ya kuyafanikisha mapinduzi yaliyoung'oa  utawala  wa  dikteta  Fulgencio  Batista  mnamo mwaka  wa 1959. Hatua alizochukua ikiwa pamoja  na  kuleta mageuzi katika sera  ya  ardhi  na  kutaifisha viwanda na  makampuni , zilisababisha uadui  kati yake  na  Marekani.
Marekani  ilijibu kwa kuiwekea  Cuba  vikwazo vya  kibiashara.  Hata  hivyo  Cuba
ilipata misaada  mikubwa  kutoka Umoja  wa kisoviet na hivyo  kuwa tegemezi wakati  wote.  Kisiwa cha Cuba kiliingia katika kipindi kigumu sana cha matatizo ya kiuchumi  baada ya Umoja  wa kisoviet kusambaratika mnamo mwaka wa 1990 .Hata hivyo mfumo wake wa kikomunisti uliweza kukihimili kipindi hicho hadi hivi karibuni ambapo Cuba na Marekani zilirejesha uhusiano wa kibalozi baina yao.
Rais wa Venezuela Nicholas Maduro amemsifu Fidel Castro kwa uongozi wake. Nae kiongozi wa zamani wa urusi Mikhael Gorbachev amemsifu Castro kwa kuiimarisha Cuba.

Hakuna maoni: