Tafuta katika Blogu Hii
Alhamisi, 3 Novemba 2016
Kiongozi wa IS asema hakuna kusalimu amri
Wakati vikosi vya Iraq vikizidi kuusogelea mji wa Mosul, kiongozi wa
wapiganaji wa kundi linalojiita Dola la Kiislamu IS Abu Bakr al-Baghdadi
amewatumia ujumbe wa sauti wapiganaji wake akiwataka kutosalimu amri
dhidi ya majeshi ya serikali. Kiongozi huyo amesikika akisema "hakuna
kusalimu amri" na kuwaambia wapiganaji kwamba ni heshima kuilinda ardhi
hiyo kuliko kusalimu amri kwa aibu. Huo ni ujumbe wa kwanza kutolewa na
kiongozi katika kipindi cha mwaka mmoja na kumekuwa na tetesi juu ya
afya na harakati za kiongozi huyo lakini hajulikani alipo. Mwezi Juni
mwaka 2014, alijitokeza hadharani mjini Mosul na kutangaza Dola la
Kiislamu nchini Iraq na Syria. Muungano wa kijeshi unaoongozwa na
Marekani na unaovinga mkono vikosi vya Iraq, unakadiria kuwepo kiasi ya
wapiganaji 3000 hadi 5000 wa IS ndani ya mji wa Mosul.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni