Tafuta katika Blogu Hii
Alhamisi, 3 Novemba 2016
Wikileaks yachapisha barua pepe mpya kuhusu Clinton
Mtandao wa Wikileaks umechapisha barua pepe mpya kutoka kwa mkuu wa timu
ya kampeni ya Hillary Clinton, John Podesta. Barua pepe hizo
zinaonyesha wizara ya mambo ya nje ikimueleza Clinton juu ya ripoti
inayohusu taarifa za matumizi ya barua pepe binafsi. Katika taarifa
zilizoko ndani ya barua pepe za Clinton, kunaonekana kuwepo na uratibu
wa karibu kati ya wizara na timu ya kampeni ya Hillary Clinton na
zinapendekeza kwamba huenda afisa wa serikali alimdokeza Bi. Clinton
kuwa taarifa zake za matumizi ya barua pepe binafsi ziko karibu
kujulikana. Timu ya kampeni ya Clinton inaishutumu Wikileaks kwa kutumia
taarifa zilizodukuliwa na Urusi katika jitihada za kuingilia uchaguzi
wa nchi hiyo. Wagombea wote wawili Donald Trump wa Republican na Hillary
Clinton wa Democrats wameendelea kutupiana vijembe katika kampeni za
lala salama kabla ya kufanyika kwa uchaguzi.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni